Rwanda yakanusha kuwasaidia waasi wa Burundi (Sauti)
Feb 11, 2016 14:46 UTC
Kwa mara ya kwanza tangu Rwanda iliposhutumiwa na Umoja wa Mataifa kuwa inawaunga mkono waasi ambao Burundi inasema wanahatarisha usalama wake, serikali ya Kigali imekanusha rasmi madai hayo
Rwanda imesema, kutokana na kuwa Burundi hivi sasa imeelemewa na matatizo yake ya ndani, ni wazi kwamba inatafuta mtu wa kumsingizia na kumbebesha lawama.
Kauli hiyo imetolewa mjini Kigali na Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda, Bi Louise Mushikiwapo ambaye pia ni msemaji wa serikali ya nchi hiyo.
Ingia kwenye picha hapo juu kusikiliza ripoti ya mwandishi wetu Sulvanus Karemera
Tags