Waislamu Nigeria wakumbuka miaka 9 tangu mauaji ya Zaria
https://parstoday.ir/sw/news/africa-i120242-waislamu_nigeria_wakumbuka_miaka_9_tangu_mauaji_ya_zaria
Harakati ya Kiislamu nchini Nigeria imeadhimisha mwaka wa 9 tangu mauaji ya Zaria, ikitoa wito wa kufunguliwa mashtaka wahusika wa mashambulizi mabaya dhidi ya Waislamu wa Shia.
(last modified 2024-12-16T23:25:19+00:00 )
Dec 16, 2024 23:25 UTC
  • Waislamu Nigeria wakumbuka miaka 9 tangu mauaji ya Zaria

Harakati ya Kiislamu nchini Nigeria imeadhimisha mwaka wa 9 tangu mauaji ya Zaria, ikitoa wito wa kufunguliwa mashtaka wahusika wa mashambulizi mabaya dhidi ya Waislamu wa Shia.

Harakati hiyo imekariri wito huo wa kufunguliwa mashitaka kwa watekelezaji wa mauaji ya Desemba 12, 2015 huko Zaria, jimbo la Kaduna.

Wito huo umetolewa huku harakati hiyo ikiadhimisha miaka 9 tangu kutokea kwa mauaji hayo ya kutisha.

Katika hotuba yake, Sheikh Ibraheem Zakzaky, kiongozi wa Harakati ya Kiislamu Nigeria ametuma salamu za rambirambi kwa wale wote waliopoteza wapendwa wao wakati wa mauaji ya Disemba 2015 na mauaji yaliyofuata.

Alieleza kwa kina jinsi serikali zilizopita nchini humo zilijaribu mafanikio kusambaratisha harakati hizo kwa kutekeleza mauaji na kumlenga yeye binafsi.

Pia aliangazia matukio mbalimbali ya kupuuza kwa wazi sheria kwa mikono tofauti ya jimbo la Nigeria katika kuwakandamiza kaka na dada wa harakati hiyo.

"Ninapongeza uthabiti wa ndugu na dada zetu wa harakati ambao wamestahamili viwango mbalimbali vya vitisho na ukandamizaji kutoka kwa serikali ya Nigeria, vikosi vyake vya usalama, na, wakati mwingine, mahakama," alisema.

Sheikh Ibrahim Zakzaky na mke wake, Mallimah Zeenah walitiwa nguvuni tarehe 13 Disemba mwaka 2015 katika shambulizi lililofanywa na jeshi la Nigeria dhidi ya kituo cha kidini cha Baqiyyatullah katika mji wa Zaria na walikuwa mahabusu kwa kipindi cha miaka 6 iliyopita kabla ya kuachiliwa huru mwezi Julai mwaka 2021.

Katika tukio hilo Jeshi la Nigeria liliua kwa umati karibu wafuasi zaidi ya 1000 wa Harakati ya Kiislamu inayoongozwa na Sheikh Ibrahim Zakzaky wakiwemo wanawe watatu na baadaye kuwazika katika makaburi ya umati.