Idadi ya miili iliyotolewa kwenye mgodi wa dhahabu Afrika Kusini yafikia 78
Mamlaka ya Afrika Kusini imefanikiwa kupata miili 78 kutoka kwenye machimbo ya dhahabu yaliyogurwa huko Stilfontein, baada ya mzingiro wa wiki kadhaa uliolenga wachimbaji haramu.
Waokoaji wa Afrika Kusini wamemaliza na kukamilisha zoezi la kumtafuta mtu yeyote aliyesalia kwenye machimbo haramu ya dhahabu ambapo takriban watu 78 wamekufa wakati wa mzingiro wa polisi, huku mfanyakazi wa kujitolea wa eneo hilo akielezea hofu ya kutoa miili yao kutoka chini ya ardhi.
Polisi walikuwa wameuzingira mgodi huo tangu Agosti mwaka jana na kukata chakula na maji ili kujaribu kuwalazimisha wachimbaji hao wakamatwe, na kusababisha kile chama cha wafanyakazi cha GIWASU kilichokiita mauaji mabaya zaidi yaliyofadhiliwa na serikali tangu kumalizika kwa ubaguzi wa rangi.
Wachimba madini haramu, wanaojulikana kama "zama zamas", wanafanya kazi katika migodi iliyogurwa na sekta ya madini inayodorora ya Afrika Kusini. Watu hao wanafanya kazi bila vibali, mara nyingi katika hali na mazingira hatari, ili kuchimba mabaki ya dhahabu. Shughuli zao zimezua ukosoaji kwa madai kwamba zinachochea mitandao ya uhalifu na kuzidisha jinai katika maeneo jirani.
Mwishoni mwa mwaka wa 2023, polisi walianzisha operesheni ya kukomesha kabisa sekta hiyo katika ukanda wa uchimbaji madini wa kaskazini-mashariki mwa Afrika Kusini, na kuzuia vifaa muhimu ili kuwalazimisha watoto kuondoka ndani ya migodi hiyo.