Al Shabab yamuua Mwendesha Mashtaka wa Jeshi, Puntland
https://parstoday.ir/sw/news/africa-i22147-al_shabab_yamuua_mwendesha_mashtaka_wa_jeshi_puntland
Kundi la kigaidi la al Shabab limempiga risasi na kumuua Mwendesha Mashtaka wa Jeshi katika eneo lenye mamlaka ya ndani la Puntland nchini Somalia.
(last modified 2026-02-25T03:34:48+00:00 )
Dec 26, 2016 01:03 UTC
  • Al Shabab yamuua Mwendesha Mashtaka wa Jeshi, Puntland

Kundi la kigaidi la al Shabab limempiga risasi na kumuua Mwendesha Mashtaka wa Jeshi katika eneo lenye mamlaka ya ndani la Puntland nchini Somalia.

Abdikarim Hassan Firdiye alipigwa risasi kichwani jana alipokuwa akiteremka kwenye gari lake nje kidogo ya mgahawa mmoja wa mji mkubwa zaidi wa Puntland, Bosasso.

Siku chache zilizopita pia wanachama wa kundi la al Shabab walimuua kwa kumpiga risasi Naibu wa Mkuu wa kanda hiyo na vilevile Naibu wa Kamanda wa Polisi ya Puntland nje ya mgahawa mmoja.

Wapiganaji wa kundi la al Shabab wanaendelea kufanya mauaji ya kigaidi Somalia

Ripoti zinasema Mwendesha Mashtaka wa Jeshi katika eneo lenye mamlaka ya ndani la Puntland, Abdikarim Hassan Firdiye amepigwa risasi kichwani na vijana wawili ambao walitoweka haraka baada ya uhalifu huo.

Msemaji wa kundi la kigaidi la al Shabab Abdiasis Abu Musab ametangaza kuwa, kundi hilo limehusika na mauaji hayo na kudai kuwa, Abdikarim Hassan Firdiye aliwahukumu kifo wapiganaji wengi wa al Shabab.