Asasi za kiraia zatahadharisha juu ya kuendelea hali mbaya ya wakimbizi Chad
https://parstoday.ir/sw/news/africa-i29882-asasi_za_kiraia_zatahadharisha_juu_ya_kuendelea_hali_mbaya_ya_wakimbizi_chad
Asasi zisizo za kiserikali zimeonya kuhusiana na kuendelea kuwa mbaya hali ya wakimbizi na mgogoro wa kibinadamu nchini Chad.
(last modified 2026-01-14T08:12:18+00:00 )
Jun 01, 2017 02:50 UTC
  • Asasi za kiraia zatahadharisha juu ya kuendelea hali mbaya ya wakimbizi Chad

Asasi zisizo za kiserikali zimeonya kuhusiana na kuendelea kuwa mbaya hali ya wakimbizi na mgogoro wa kibinadamu nchini Chad.

Taarifa ya asasi hizo imeeleza kuwa, wakimbizi huko Chad wanakabiliwa na hali mbaya ya kibinadamu na kwamba, kuna haja ya kuchukuliwa hatua za haraka za kuwasaidia ili kuepusha kutokea maafa ya kibinadamu.

Pierre Valiquette, mkuu wa moja ya asasi za kiraia nchini Chad sambamba na kutahadharisha kuhusiana na kuendelea mgogoro wa wakimbizi huko Chad amesema kuwa, takribani wakimbizi wote walioko nchini humo wanahitajia misaada ya kibinadamu hususan chakula. 

Hivi karibuni Umoja wa Mataifa ulitangaza kuwa, kumetengwa bajeti maalumu ya kuwasaidia wakazi wa eneo la Ziwa Chad ambao kwa sasa wanakabiliwa na hali mbaya kimaisha.

Stephen O'Brien, Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya kibinadamu

O'Brien, Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya kibinadamu na mratibu wa misaada ya kibinadamu amesema kuwa, umoja huo umetenga bajeti ya dola  3.5 kwa ajili ya kuwasaidia wakazi wa Ukanda wa Ziwa Chad wanaotatizika kudhamini mahitaji yao ya lazima ya kila siku.

Kwa mujibu wa takwimu za Umoja wa Mataifa watu milioni 11 katika eneo la Ziwa Chad linalojumuisha Cameroon, magharibi mwa Chad, kusini mashariki mwa Niger na kaskazini mashariki mwa Nigeria wanahitajia misaada ya haraka ya chakula.