Mlipuko wa kipindupindu waua makumi Cameroon na Nigeria
https://parstoday.ir/sw/news/africa-i54719-mlipuko_wa_kipindupindu_waua_makumi_cameroon_na_nigeria
Makumi ya watu wamefariki dunia kutokana na ugonjwa wa kipindupindu kaskazini mwa Cameroon tokea mwanzoni mwa mwaka huu hadi sasa.
(last modified 2023-11-27T08:44:11+00:00 )
Jul 12, 2019 20:37 UTC
  • Mlipuko wa kipindupindu waua makumi Cameroon na Nigeria

Makumi ya watu wamefariki dunia kutokana na ugonjwa wa kipindupindu kaskazini mwa Cameroon tokea mwanzoni mwa mwaka huu hadi sasa.

Kwa mujibu wa taarifa ya Wizara ya Afya ya nchi hiyo, watu 93 wamefariki dunia huku wengine zaidi ya elfu moja wakiambukizwa ugonjwa huo ndani ya mwaka huu 2019 pekee nchini humo.

Huku hayo yakiripotiwa, watu watatu wapoteza maisha katika jimbo la Adamawa nchini Nigeria kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu. 

Hayo yamesemwa na  Dakta Bwalki Dalili, Mkurugenzi wa Taasisi ya Ustawi wa Jamii wa Adamawa ambaye ameongeza kuwa, watu  244 wameambukizwa ugonjwa huo.

Jimbo la Adamawa nchini Nigeria linalokabiliwa na kipindipindu 

Dalili amesema wamechukua hatua stahiki kuzuia kuenea kwa ugonjwa huo katika maeneo mengine ya nchi hiyo ya magharibi mwa Afrika.

Ugonjwa wa kipindupindu husababishwa na baktria waitwao Vibrio cholera na huenezwa kwa kunywa maji yasiyo salama. Dalili za ugonjwa huo ni maumivu ya tumbo, kuharisha, kutapika pamoja na homa.