AU na UN zalaani mapigano mapya Jamhuri ya Afrika ya Kati + Sauti
Sep 15, 2019 12:11 UTC
Umoja na Mataifa na Umoja wa Afrika zimelaani vikali kitendo cha kuibuka upya mapigano katika mji wa Birao wa kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Afrika ya Kati kwenye mpaka na Sudan Kusini. Mapigano hayo yaliyoyahusisha makundi mawili hasama ya genge la Seleka, yamepelekea makumi ya watu kuuawa na wengine wengi kujeruhiwa. Hii ni katika hali ambayo makundi hayo, yalitia saini mkataba wa amani kwenye serikali ya umoja wa kitaifa nchini CAR. Mwandishi wetu Mossi Mwasi na maelezo zaidi...
Tags