Rais Samia awatahadharisha Watanzania dhidi ya Corona
https://parstoday.ir/sw/news/africa-i70806-rais_samia_awatahadharisha_watanzania_dhidi_ya_corona
Rais Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania waendelee kuchukua tahadhari za kujikinga na ugonjwa wa Covid-19 unaosababishwa na virusi vya Corona.
(last modified 2025-10-20T07:03:11+00:00 )
Jun 02, 2021 04:25 UTC
  • Rais Samia awatahadharisha Watanzania dhidi ya Corona

Rais Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania waendelee kuchukua tahadhari za kujikinga na ugonjwa wa Covid-19 unaosababishwa na virusi vya Corona.

Kwa mujibu wa gazeti la Mwananchi, Rais Samia alitoa mwito huo jana Jumanne, Juni Mosi, alipofanya ziara ya kushtukiza katika Hospitali Rufaa ya Mkoa Mwananyamala jijini Dar es Salaam.

Amesema baadhi Watanzania wanaziba midomo  kwa kutumia barakoa na vifaa vingine lakini wengine hawafanyi hivyo, hali inayowaweka kwenye hatari kubwa hivyo ni vema kila mmoja akafanya jitihada za kujikinga.

Mama Samia ameeleza bayanakuwa,  “Sasa hivi tuko vizuri, lakini mnasikia wenzetu huko India mambo yanavyowapukutisha watu wamechoma hadi kuni hamna kwahiyo desturi ya mambo haya yanaambukiza na yakitoka sehemu moja yanaenda sehemu nyingine."

Mama Samia akiwa amevalia barakoa alipokutana na wakuu wa Kamati ya Corona Tanzania

Amebainisha kuwa, “Tumejitahidi kuzuia usafiri wa kutoka kule kuja huku au hapa  kwenda kule ili virusi visije, kwahiyo kila mtu achukue tahadhari pale alipo, kama ni kunawa mikono na kwa bahati mbaya anayekuja nacho humjui,”amesema.

Rais wa Tanzania ameongeza kkuwa, “Tumepokea vya aina yote  sijui cha South Afrika, sijui vya wapi sasa hivi kuna vya India, kila mtu achukue tahadhari pale alipo kama ni kunawa mikono kujikinga ili tuepukane na lile balaa kubwa.”