Makumi ya wanamgambo wa Boko Haram watiwa nguvuni Nigeria
Duru za kijeshi za Cameroon zimearifu kuwa makumi ya wanamgambo wa kitakfiri wa Boko Haram wametiwa mbaroni katika oparesheni ya kijeshi iliyofanywa na jeshi la Cameoon kaskazini mashariki mwa Nigeria.
Duru za kijeshi za Cameroon zimetangaza kuwa makumi ya wanamgambo wa kundi la kigaidi la Boko Haram wametiwa nguvuni katika mji wa Gambaru kaskazini mashariki mwa NIgeria kufuatia oparesheni iliyofanywa na wanajeshi wa Cameroon wanaohudumu kwenye kikosi cha mataifa kadhaa ya kamisheni ya Ukanda wa Ziwa Chad (CBLT) na kwa kushirikiana na jeshi la Nigeria. Oparesheni hiyo mpya ya kijeshi ilitekelezwa jana Jumatano baada ya Boko Haram Ijumaa iliyopita kuishambulia kambi moja ya kijeshi katika eneo la Bosso kusini mashariki mwa Niger na kuuwa wanajeshi wa nchi hiyo 32 na wawili wa Nigeria. Wanajeshi wengine 67 walijeruhiwa katika shambulio hilo. Kundi la boko Haram limeshadidisha mashambulizi yake huko kaskazini mashariki mwa Nigeria, licha ya viongozi wa nchi hiyo kutangaza kuwa kundi hilo limedhoofika.