-
Ndoto ya Afrika isiyo na mpaka yakaribia baada ya Togo kuruhusu Waafrika kuingia nchini humo bila visa
May 22, 2026 03:58Togo imetangaza ruhusa kwa raia wa nchi zote za Afrika kuingia nchini humo bila visa na kukaa huko kwa hadi siku 30, mradi tu wawasilishe maombi kielektroniki kupitia jukwaa la serikali, saa 24 kabla ya kuwasili nchini Togo.
-
Jumuiya ya Nchi za Kiarabu yakemea mpango wa ‘Somaliland’ kufungua ubalozi katika al-Quds inayokaliwa kwa mabavu
May 21, 2026 13:00Jumuiya ya Nchi za Kiarabu (Arab League) imekosoa vikali uamuzi wa eneo la Somaliland lililojitenga na Somalia wa kufungua ubalozi katika mji mtakatifu wa al Quds (Jerusalem) unaokaliwa kwa mabavu na utawala wa Israel, ikisema hatua hiyo “haikubaliki kabisa.”
-
Ebola imeua watu 139, wengine 600 wameambukizwa DRC na Uganda
May 21, 2026 12:56Takriban wagonjwa 600 sasa wanashukiwa kuwa na Ebola na vifo 139 vikishukiwa kusababishwa na ugonjwa huo hali inayoongeza hofu ya kuenea zaidi kwa mlipuko wa sasa wa Ebola.
-
UNICEF: Mlipuko wa Ebola umewaweka Watoto hatarini
May 21, 2026 04:33Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF, limesema lina wasiwasi mkubwa kuhusu mlipuko wa Ebola unaoendelea katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo DRC na Uganda, huku likionya kuwa watoto wako kwenye hatari kubwa zaidi.
-
Rwanda yaimarisha udhibiti wa mpakani kutokana na mlipuko hatari wa Ebola nchini Kongo
May 20, 2026 10:58Mamlaka ya Rwanda imeongeza hatua za uchunguzi wa afya na kuimarisha udhibiti katika mpaka na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo huku mlipuko hatari wa homa ya Ebola ukiendelea kuitatiza Kongo.
-
Uganda yawaweka karantini zaidi ya watu 100 huku WHO ikitoa tahadhari kuhusu kasi ya Ebola
May 20, 2026 03:20Serikali ya Uganda inasema zaidi ya watu 100 wamewekwa karantini huku maafisa wa afya wakijitahidi kudhibiti mlipuko nadra wa Ebola unaohusishwa na aina ya virusi vya Bundibugyo.
-
Sheikh Zakzaky: Damu ya Imam Khamenei aliyeuawa shahidi itawaandama Wazayuni
May 20, 2026 02:55Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu nchini Nigeria amesema Imam Ali Khamenei aliyeuawa shahidi na damu yake safi vitaendelea kuuandama utawala wa Kizayuni wa Israel ambao ni sawa na donda la saratani.
-
Serikali ya Uganda yaweka udhibiti wa mipaka kutokana na mlipuko wa Ebola DRC
May 19, 2026 12:44Uganda imeanzisha udhibiti wa mipaka kutokana na mlipuko wa virusi vya Ebola. Wafanyakazi wa afya nchini humo tayari wameanza kupima halijoto ya watu huku wakiwasaidia kunawa mikono yao karibu na Bundibugyo magharibi mwa Uganda.
-
ICC yasikiliza kesi dhidi ya kamanda wa zamani wa Gereza la Mitiga huko Libya kuhusu unyanyasaji
May 19, 2026 11:12Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) imefungua kesi dhidi ya kamanda wa zamani wa gereza la Libya, Mohammed Ali El Hishri, anayetuhumiwa kusimamia uhalifu dhidi ya ubinadamu katika kituo maarufu cha kizuizi cha Mitiga karibu na Tripoli.
-
Mgomo wa sekta ya uchukuzi Kenya waahirishwa kuruhusu mazungumzo baina ya serikali na sekta hiyo
May 19, 2026 11:02Mgomo wa sekta ya uchukuzi uliokuwa umeingia siku ya pili nchini Kenya umeahirishwa kwa muda wa siku saba ili kutoa nafasi kwa mazungumzo kati ya serikali na viongozi wa sekta hiyo.