-
Kuuzuliwa Spika wa Baraza la Wawakilishi la Marekani: Jambo ambalo halijawahi kutokea
Oct 05, 2023 04:48Kevin McCarthy, Spika wa Bunge la Wawakilishi la Marekani kutoka chama cha Republican juzi Jumanne aliuzuliwa na wabunge wa bunge hilo katika vuta nikuvute kati ya wabunge wa chama cha Republican wenye siasa kali na wenye msimamo wa wastani.
-
Kufukuzwa makumi ya wanadiplomasia wa Canada nchini India
Oct 04, 2023 22:50Siku ya Jumanne, serikali ya India iliitaka serikali ya Canada kuwaondoa wanadiplomasia wake wengine 40 kutoka nchi hiyo. Takwa hilo la kufukuzwa idadi kubwa ya wanadiplomasia wa Canada linaonyesha kuongezeka mvutano katika uhusiano wa nchi mbili.
-
Kutomwamini Netanyahu Ben Gvir; mgawanyiko mpya katika baraza la mawaziri la Israel
Oct 04, 2023 04:21Gazeti la Yediot Aharonot limeripoti kuwa Benjamin Netanyahu, Waziri Mkuu wa utawala haramu wa Israel hamwaliki tena Itamar Ben Gvir, Waziri wa Usalama wa Ndani kwenye vikao vya siri ya juu vya kiusalama vya utawala huo.
-
Kitendo cha al-Ittihad mjini Isfahan; kuchanganywa mechi ya mpira wa miguu na masuala ya kisiasa
Oct 04, 2023 02:41Katika kitendo kisicho cha uanamichezo siku ya Jumatatu, timu ya mpira wa miguu ya Saudi Arabia iliamua kutoingia kwenye uwanja wa Naqshe Jahan kwa ajili ya kuchuana na timu ya Sepahan ya mjini Isfahan.
-
Mtazamo wa Kiongozi Muadhamu: Mchezo wa kamari wa kuanzisha uhusiano wa kawaida na Israel utashindwa
Oct 03, 2023 22:58Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa, mchezo wa kamari wa kuanzisha uhusiano wa kawaida na utawala wa Kizayuni ni mithili ya kubeti juu ya farasi asiyeshinda katika mashindano, kwa sababu leo hii harakati ya Wapalestina iko hai na ina utayari zaidi kuliko wakati mwingine wowote, na utawala wa Kizayuni unaelekea katika kifo.
-
Umoja wa Kiislamu maandalizi ya kuhuisha adhama ya ustaarabu wa Kiislamu
Oct 03, 2023 09:55Mkutano wa 37 wa Kimataifa wa Umoja wa Kiislamu umefanyika hapa mjini Tehran. Kama ilivyo ada, mkutano wa kila mwaka wa kimataifa wa Umoja wa Kiislamu umefanyika hapa Tehran kwa mnasaba wa Wiki ya Umoja sambamba na Maulidi ya Mtume (saww).
-
Kutoka mapambano ya silaha katika Ukingo wa Magharibi hadi kuanza tena maandamano ya haki ya kurejea wakimbizi huko Gaza.
Oct 02, 2023 23:13Ikiwa ni katika muendelezo wa walowezi wa Kizayuni kuvunjia heshima Msikiti wa Al-Aqswa, siku ya Jumapili asubuhi walowezi hao walifanya vitendo vya uchochezi katika eneo hilo takatifu kwa kuingia humo kinyume cha sheria, ambapo walowezi wa mrengo wa kulia waliimba na kucheza densi kwenye lango la msikiti huo mtukufu.
-
Uturuki bado inatafuta fursa kwa kuendelea kukalia ardhi ya Syria
Oct 02, 2023 07:35Ankara imetangaza kwa mara nyingine kuwa serikali ya Uturuki itaanzisha tena mazungumzo yake na Iran na Russia kwa lengo la kuboresha uhusiano na Syria.
-
Kutoka muqawama wa silaha katika Ukingo wa Magharibi hadi kuanza tena kwa maandamano ya haki ya kurejea wakimbizi huko Gaza
Oct 02, 2023 04:26Katika muendelezo wa vitendo vya walowezi wa Kizayuni vya kuuvunjia heshima Msikiti wa Al-Aqswa katika siku chache zilizopita kwa kisingizio cha sikukuu za Kiyahudi, Jumapili asubuhi ya jana, watu hao walifanya vitendo vya uchochezi katika eneo hili takatifu baada ya kuingia humo kinyume cha sheria. Walowezi wa Kizayuni wa mrengo wa kulia walianza kucheza, kurukaruka huku wakiimba kwenye lango la Msikiti wa Al-Aqsa.
-
Ombi la Qatar kwa Umoja wa Mataifa la kujiunga utawala wa Kizayuni wa Israel na mkataba wa NPT
Oct 01, 2023 22:59Qatar imeutaka utawala ghasibu wa Israel ujiunge na mkataba wa kupiga marufuku uenezaji wa silaha za nyuklia duniani NPT.