Mokhber: Mkakati wa Iran wa kuunga mkono Muqawama hautabadilika baada ya kufa shahidi Sayyid Raisi
Rais wa muda wa Iran amesema stratejia kuu ya Jamhuri ya Kiislamu katika kutoa msukumo na uungaji mkono kwa vuguvugu la Muqawama hususan kwa makundi ya Muqawama ya Palestina haitabadilika kwa sababu ya mabadiliko ya watu.
![](https://media.parstoday.ir/image/4bxx6a29325f551smcm_800C450.jpg)
Kwa upande wake, Ziyad Al-Nakhalah ametoa mkono wa pole kwa Serikali na wananchi wa Iran kwa tukio la kufa shahidi Rais Sayyid Ebrahim Raisi na Waziri wa Mambo ya Nje Hossein Amir-Abdollahian, pamoja na maafisa wengine waliokufa shahidi pamoja nao na kueleza kwamba Jamhuri ya Kiislamu ya Iran itaushinda na kuuvuka msukosuko huu kutokana na kubarikiwa kuwa na Kiongozi mkubwa, maafisa wenye uwezo unaostahiki na wananchi wenye mawazo na fikra za kimapinduzi.
Helikopta iliyokuwa imembeba Sayyid Ebrahim Raisi, Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Jumapili jioni Mei 19, 2024 ilipata ajali ilipokuwa ikirejea kutoka kwenye hafla ya ufunguzi wa bwawa la Qiz Qalasi kwenye mpaka wa pamoja wa Iran na Jamhuri ya Azerbaijan.
Wakati helikopta hiyo ilipokuwa inaelekea mji wa Tabriz, ilianguka katika eneo la Varzghan mkoani Azarbaijan Mashariki, kaskazini-magharibi mwa Iran. Ndani yake walikuwemo pia Hossein Amir-Abdollahian, Waziri wa Mambo ya Nje, Imam wa Ijumaa wa Tabriz, Gavana wa Azarbaijan Mashariki na watu wengine; na wote pamoja wakaifika hadhi tukufu ya kufa shahidi.../