Iran iko tayari kwa ajili ya uchaguzi wa 19 Mei
https://parstoday.ir/sw/news/iran-i26704-iran_iko_tayari_kwa_ajili_ya_uchaguzi_wa_19_mei
Makamu wa Kwanza Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema serikali imejitayarisha kikamilifu kwa ajili ya kuandaa uchaguzii wa rais na uchaguzi mdogo wa bunge tarehe 19 Mei.
(last modified 2023-11-27T08:44:11+00:00 )
Mar 22, 2017 03:25 UTC
  • Iran iko tayari kwa ajili ya uchaguzi wa 19 Mei

Makamu wa Kwanza Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema serikali imejitayarisha kikamilifu kwa ajili ya kuandaa uchaguzii wa rais na uchaguzi mdogo wa bunge tarehe 19 Mei.

Akizungumza Jumatano alipotembelea makao makuu ya Idara ya Uchaguzi mkoani Kerman kusini mashariki mwa Iran, Is'haq Jahangiri amesisitiza kuwa, uchaguzi  nchini Iran unazingatiwa kieneo na kimataifa.

Huku akiashiria hali nyeti katika eneo la Asia Magharibi na nara tata zinazotolewa na baadhi ya watawala wa Ulaya na Marekani amesema, kushiriki kwa wingi wananchi katika uchaguzi huu ni jambo litakaloonyesha nguvu na uwezo wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Iran amesema kuna ushirikiano mzuri baina ya idara ya uchaguzi na wasimamizi wa uchaguzi. 

Uchaguzi wa rais wa awamu ya 12 na uchaguzi wa duru ya tano ya mabaraza ya Kiislamu ya miji na vijiji na pia uchaguzi mdogo wa 10 wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu, Bunge la Iran, utafanyika kwa pamoja Ijumaa tarehe 19 Mei mwaka huu.