Iran kuzindua satalaiti tatu mpya za Zafar, Pars 1 na Nahid 1
https://parstoday.ir/sw/news/iran-i56431-iran_kuzindua_satalaiti_tatu_mpya_za_zafar_pars_1_na_nahid_1
Mkuu wa Shirika la Anga za Mbali la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema Iran itakamilisha utengenezaji wa satalaiti tatu mpya katika kipindi cha miezi mitatu ijayo.
(last modified 2023-11-27T08:44:11+00:00 )
Oct 05, 2019 04:33 UTC
  • Iran kuzindua satalaiti tatu mpya za Zafar, Pars 1 na Nahid 1

Mkuu wa Shirika la Anga za Mbali la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema Iran itakamilisha utengenezaji wa satalaiti tatu mpya katika kipindi cha miezi mitatu ijayo.

Dakta Murtadha Barari ameyasema hayo leo Jumamosi mjini Tehran wakati akizungumza na waandishi habari kwa munasaba wa kuanza Wiki ya Kimataifa ya Anga za Mbali. Amesema utengenezaji wa satalaiti tatu mpya utakamilika katika kipindi cha miezi mitatu ijayo na baadaye kurushwa katika anga za mbali. Amezitaja satalaiti hizo kuwa ni Zafar, Pars 1 na Nahid 1.

Akiashiria kufeli baadhi ya sataliti ambazo Iran imezirusha katika anga za mbali, Mkuu wa Shirika la Anga za Mbali la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, kwa mujibu wa takwimu za kimataifa, katika miaka 3 ya kwanza ya Marekani kuanza harakati zake katika anga za mbali, sataliti zake 27 kati ya 43 ilizorusha katika anga za mbali zilifeli.

Satalaiti ya kwanza ya Iran ya Omid ilirushwa katika anga za mbali kwa kutumia chombo cha kubebea satalaiti ya Safir

Ameongeza kuwa, sataliti 5 kati ya 11 ambazo Russia pia mwanzoni ilituma katika anga za mbali zilifeli. Dkt. Barari amesema kuwa, kwa mujibu wa takwimu asilimia 40 ya satalaiti za Iran zimefanikiwa kufika katika anga za mbali.

Iran ilirusha katika anga za mbali satalaiti yake ya kwanza kabisa inayojulikana kama Omid (yaani Tumaini) mwaka 2009. Iran pia imetangaza kuwa katika kipindi cha miaka michache ijayo itatuma mwanadamu katika anga za mbali.