Rais Rouhani: Njia pekee ya kukabiliana na wavamizi ni mapambano
Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, njia pekee ya kukabiliana na wavamizi, ni mapambano.
Rais wa Iran ameyasema hayo Jumanne katika ujumbe ambao amemtumia mwenzake wa Lebanon Michel Aoun kwa mnasaba wa ushindi wa taifa la Lebanon dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel mwaka 2000
Amesema kukombolwa maeneo ya kusini mwa Lebanon ambayo yalikuwa yanakaliwa kwa mabavu na utawala wa Kizayuni wa Israel miaka 21 iliyopita ni ushindi uliojaa fakhari kwa taifa la Lebanon.
Rouhani amesema ushindi huo ulionyesha wazi kuwa njia pekee ya kukabiliana na wavamizi ni mataifa kusimama kidete na kupambana.
Rais Rouhani halikadhalika amesema Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inafungamana na taifa na serikali ya Lebanon katika kulinda umoja na mipaka ya nchi hiyo.
Kila mwaka mwezi 25 Mei, Lebanon huadhimisha kumbukumbu ya kuondoka kwa madhila wanajeshi vamizi wa Isrel katika ardhi zake za kusini. Siku hii nchini Lebanon hujulikana kama Siku ya Kitaifa ya Mapambano na Ukombozi.