-
'Nchi inayoshiriki mauaji ya kimbari Gaza inataka kusafisha sura yake chafu kwa kuandaa Kombe la Dunia 2026'
Jun 12, 2026 13:52Nyota wa zamani wa soka wa Misri na mchambuzi wa masuala ya michezo, Mohamed Aboutrika, ameibua wimbi kubwa la majibizano na mijadala kwenye mitandao ya kijamii, baada ya kukosoa sera za undumakuwili katika kuandaa mashindano makubwa ya michezo, na jitihada za baadhi ya nchi za kutumia michezo kama wenzo wa kutakasa na kusafisha sura zao chafu za kisiasa.
-
Rais Pezeshkian: Wairani wameungana kuilinda nchi yao dhidi ya vitisho
Jun 12, 2026 12:44Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, amesema kwamba taifa litalinda uhuru na mamlaka yake ya kitaifa licha ya kuongezeka vitisho na mashinikizo.
-
Rais wa Nigeria atangaza mauaji ya wapiganaji 13,000 mwaka jana
Jun 12, 2026 12:36Rais wa Nigeria, Bola Ahmed Tinubu, ametangaza leo Ijumaa kwamba "magaidi" wasiopungua 13,000 waliuawa nchini Nigeria mwaka jana, akisisitiza kwamba idadi ya vifo vinavyotokana na uasi wa kutumia silaha nchini humo imepungua kwa 81% tangu alipochukua madaraka Mei 2023.
-
Handala yadukua mifumo ya maji ya California baada ya Marekani kushambulia maghala ya maji ya Iran
Jun 12, 2026 11:23Kundi la wadukuzi wanaopinga uvamizi wa kivita wa Marekani limetangaza kwamba limedukua vituo vya maji vya California kama kulipiza kisasi cha moja kwa moja kwa shambulio la anga la Marekani lililoharibu maghala ya maji ya kunywa kusini mwa Iran.
-
Iran: Makubaliano ya kumaliza vita yanakaribia lakini Marekani ina misimamo kinzani na inaendeleza uchokozi
Jun 12, 2026 04:45Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa sehemu muhimu za maelewano yanyolenga kumaliza vita vilivyolazimishwa zinakaribia kukamilika, pamoja na kuwepo misimamo kinzani ya Washington na vitendo vya mara kwa mara vya uchokozi wa kijeshi vinavyolenga kuvuruga mchakato wa kidiplomasia.
-
Rais wa Colombia aishambulia Israel katika Baraza la Usalama la UN, asema ni utawala wa kinazi
Jun 12, 2026 04:44Rais wa Colombia, Gustavo Petro, ameifananisha Israel na "utawala wa Nazi" katika maoni yake kuhusu vita vya kuangamiza vya Tel Aviv katika Ukanda wa Gaza.
-
Kwa mara ya kwanza katika muongo mmoja, idadi ya wakimbizi duniani ilipungua mwaka 2025
Jun 12, 2026 04:41Kamisheni Kuu ya Wakimbizi ya Umoja wa Mataifa (UNHCR) imetangaza kwamba idadi ya watu waliolazimika kuhama makwao duniani kote ilipungua mwaka wa 2025, ikiwa ni mara ya kwanza kurekodiwa punguo kama hilo katika muongo mmoja, licha ya viwango vya juu vya wakimbizi wa muda mrefu.
-
Ujenzi wa kituo cha Ebola cha Marekani nchini Kenya unaendelea kwa kasi
Jun 12, 2026 04:38Licha ya amri ya Mahakama Kuu ya Kenya ya kusimamisha ujenzi wa kituo cha karantini cha kuwapokea raia wa Marekani wanaoshukiwa kuwa na Ebola na maandamano ya Wakenya wenye hasira huko Nanyuki, ujenzi wa kituo hicho unaendelea kwa kasi ndani ya kambi ya jeshi ya Laikipia katikati mwa Kenya.
-
Ni kosa kubwa... Blatter amkosoa Infantino na Marekani kuhusu mwamuzi wa Somalia FIFA 2026
Jun 12, 2026 04:32Wakati ambapo macho yote yameelekezwa kwenye viwanja vya mashindano ya Kombe la Dunia huko Marekani, Mexico na Canada, Mswizi Joseph Blatter, rais wa zamani wa Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA), ameelekeza mishale ya hasira yake kwa mrithi wake Gianni Infantino na nchi mwenyeji mwenza Marekani, akiimbusha dunia kuwa "shujaa wa FIFA" anafuatilia mashindano hayo kwa uchungu.
-
Majeshi ya Iran yashambulia ngome za kijeshi za Marekani kujibu uchokozi
Jun 11, 2026 11:42Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) likishirikiana na Jeshi la Taifa la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran (Artesh), limetangaza mfululizo wa operesheni za kijeshi za kulipiza kisasi zilizoratibiwa vyema dhidi ya kambi za kijeshi za Marekani katika eneo la Asia Magharibi.