-
Maprofesa 12 wa Chuo Kikuu cha Amirkabir watajwa miongoni mwa 1% ya watafiti watajika sana duniani
Jun 09, 2026 04:39Maprofesa 12 wa Chuo Kikuu cha Teknolojia cha Amirkabir cha Iran wametambuliwa miongoni mwa asilimia moja bora zaidi ya watafiti waliotajwa sana duniani, kwa mujibu wa ripoti ya hivi karibuni iliyotolewa na Taasisi ya Unukuzi na Ufuatiliaji wa Sayansi ya Ulimwengu wa Kiislamu (Islamic World Science Citation and Monitoring Institute (ISC)).
-
Pezeshkian: Iran haitalegeza kamba, itasimama kidete kulinda taifa dhidi ya vitisho
Jun 09, 2026 04:37Rais Masoud Pezeshkian ametilia mkazo msimamo thabiti wa Iran dhidi ya tishio lolote, akisema Jamhuri ya Kiislamu haitarudi nyuma wala kusita kulinda usalama na amani ya taifa lake.
-
Rais wa Colombia asema 'ufashisti katika Ikulu ya White House unapofusha mantiki na akili
Jun 09, 2026 04:23Rais wa Colombia, Gustavo Petro, ameikosoa Marekani kuhusu "ufashisti ulioenea katika Ikulu ya White House" huku mvutano ukiongezeka kati ya Bogota na Washington.
-
Lavrov: Guterres anashirikiana na Magharibi, Washington haina nia ya kurudi kwenye makubaliano ya Anchorage
Jun 09, 2026 04:18Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia, Sergey Lavrov amekosoa utendaji wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, akisisitiza haja ya kutekelezwa kanuni za Mkataba wa Umoja wa Mataifa "bila kubagua".
-
Refa bora wa Afrika azuiwa kuingia Marekani licha ya kuteuliwa na FIFA kwa Kombe la Dunia
Jun 09, 2026 02:57Katika tukio jingine la kashfa siku chache kabla ya Kombe la Dunia 2026, mwamuzi mashuhuri kutoka Somalia, anayesifiwa sana kuwa miongoni mwa marefa bora zaidi barani Afrika, amezuiwa kuingia nchini Marekani.
-
Bab al-Mandab, mstari mpya wa kuzuia hujuma na kuimarisha uwiano wa "Umoja wa Medani"
Jun 08, 2026 12:10Msemaji wa Jeshi la Yemen ametangaza kwamba kuanzia sasa jeshi hilo limeanza kutekeleza amri ya kupiga marufuku kikamilifu meli zote za utawala haramu wa Israel kupita katika maji ya Bahari ya Shamu au kwa Kiingereza Red Sea na kwamba kuanzia wakati wa kutangazwa marufuku hiyo na kuendelea urambazaji wa baharini wa Israel katika Bahari Nyekundu utakuwa shabaha halali ya jeshi la wanajeshi wa Yemen.
-
Jeshi la Iran lashambulia kambi za kimkakati za anga za jeshi la anga la Israel kujibu uchokozi
Jun 08, 2026 11:23Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetangaza kuanzisha “Operesheni Nasr” (Ushindi), likisema limezilenga kambi za kimkakati za anga za utawala wa Israel za Nevatim na Tel Nof, kama hatua ya kujibu mashambulizi ya makombora yaliyolenga vituo vya rada vya Iran.
-
Araghchi afanya mazungumzo ya kidiplomasia kuhusu uchokozi wa Israel
Jun 08, 2026 11:20Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araghchi, amefanya mfululizo wa mazungumzo kwa njia ya simu na baadhi ya mawaziri wenzake wa maeneo mbali mbali duniani pamoja na kamanda wa jeshi, kufuatia hatua ya Iran kujibu ukiukaji wa mara kwa mara wa makubaliano ya usitishaji mapigano nchini Lebanon unaotekelezwa na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Yemen yatangaza marufuku ya meli za Israel katika Bahari ya Sham
Jun 08, 2026 11:13Vikosi vya Jeshi la Yemen vimetangaza marufuku kamili ya usafiri wa baharini wa Israel katika Bahari Nyekundu (Bahari ya Sham), vikisema kwamba harakati zote za adui katika eneo hilo sasa zitachukuliwa kuwa malengo halali ya kijeshi, baada ya kutekeleza shambulizi la kombora lenye usahihi dhidi ya maeneo nyeti ya Israel huko Tel Aviv.
-
Visa vya Ebola vyazidi 500 nchini DRC huku tahadhari ya kuenea zaidi ikitolewa
Jun 08, 2026 11:12Idadi ya visa vilivyothibitishwa vya ugonjwa wa Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) imefikia 515, vikiwemo vifo 91, huku mamlaka za afya zikionya kuwa maambukizi bado yanaendelea na huenda visa vikazidi kuongezeka ikiwa hatua za udhibiti hazitaimarishwa haraka.