-
Jeshi Iran lashambulia makao ya Shin Bet na vituo vya ndege za kivita Israel
Mar 12, 2026 09:32Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu limetangaza kutekeleza shambulio la droni au ndege ya kivita isiyo na rubani dhidi ya kituo cha kijeshi cha Palmachim pamoja na makao ya Shin Bet ndani ya utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Hizbullah yatwanga ngome za Israel kwa makombora na droni
Mar 12, 2026 08:15Harakati ya Hizbullah ya Lebanon imetoa taarifa mapema leo ikisema kwamba imeshambulia ngome za utawala haramu wa Israel kaskazini na katikati mwa ardhi ya Palestina inayokaliwa kwa mabavu (Israel).
-
Middle East Monitor: Vita vya Iran huenda vikawa mwisho wa kisiasa wa Netanyahu
Mar 12, 2026 08:08Tovuti ya Middle East Minitor imeandika makala ya uchambuzi kuhusu mashambulizi ya kichokozi ya Marekani na utawala wa Kziayuni wa Israel ikisema kuwa vita ambavyo Benjamin Netanyahu amejiandaa kwa ajili yake kwa miaka mingi yumkini vikapelekea kutengwa kisiasa na kuporomoka stratejia yake.
-
Seneta wa Marekani: Serikali ya Trump imesema uongo kuhusu shambulio dhidi ya shule ya Iran
Mar 12, 2026 08:05Seneta wa Marekani amekosoa uongo wa kukaririwa wa serikali na jeshi la nchi hiyo na kusema serikali imetudanganya kuhusu shambulizi lililolenga shule ya watoto wadogo nchini Iran.
-
Rais wa Iran atangaza masharti ya kusitishwa vita vya kutwishwa vya US, Israel
Mar 12, 2026 07:21Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian ametangaza masharti kadhaa ya kuhitimisha vita vya kichokozi vilivyoanzishwa na Marekani na utawala wa Kizayuni dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu; huku tawala mbili hizo za kigaidi zikiendelea kushambulia maeneo muhimu ya kiraia kama shule, hospitali, makazi ya watu, na turathi za kihistoria za nchi hii.
-
Araghchi aonya UN: Kunyamazia kimya uvamizi wa US, Israel kutashadidisha taharuki katika eneo
Mar 12, 2026 06:53Waziri wa Mambo ya Nje ya Iran amesema katika mazungumzo yake ya simu na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres kuwa, kufumbia macho au kutochukua hatua za maana mkabala wa vitendo vya kivamizi vya Marekani na Israel dhidi ya Iran kutafungua njia ya kushadidi ukosefu wa utulivu na taharuki katika eneo.
-
Iran yasema haitashiriki Kombe la Dunia la FIFA 2026
Mar 12, 2026 06:27Waziri wa Michezo wa Iran, Ahmad Donyamali amesema timu ya taifa ya soka ya Jamhuri ya Kiislamu haitashiriki katika fainali za Kombe la Dunia katika msimu ujao wa joto, licha ya Rais wa Shirikisho la Soka Duniani FIFA, Gianni Infantino kusisitiza kuwa amehakikishiwa na Rais Donald Trump wa Marekani kwamba Iran inakaribishwa kushiriki mashindano hayo makubwa zaidi ya soka duniani, pamoja na vita vinavyoendelea.
-
Korea Kaskazini yampongeza Ayatullah Mojtaba Khamenei kwa kuchaguliwa kuwa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu
Mar 12, 2026 02:50Korea Kaskazini imepongeza Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei kwa kuchaguliwa kwake kuwa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran.
-
Kamanda Hatami: Tutalinda heshima na hadhi ya Iran ya Kiislamu hadi tone la mwisho la damu
Mar 12, 2026 02:27Kamanda Mkuu Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema vijana wa ardhi hii takatifu watalinda heshima ya Iran kwa nguvu na azma hadi tone la mwisho la damu
-
Pezeshkian: Iran haina nia ya kuingia katika mzozo na nchi za eneo
Mar 12, 2026 02:24Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Masoud Pezeshkian, amesisitiza kwamba Iran haitaki vita au uhasama na nchi za eneo, bali inalenga tu vituo vinavyotumiwa kama chanzo cha mashambulizi dhidi ya ardhi yake.