-
Bab al-Mandab, mstari mpya wa kuzuia hujuma na kuimarisha uwiano wa "Umoja wa Medani"
Jun 08, 2026 12:10Msemaji wa Jeshi la Yemen ametangaza kwamba kuanzia sasa jeshi hilo limeanza kutekeleza amri ya kupiga marufuku kikamilifu meli zote za utawala haramu wa Israel kupita katika maji ya Bahari ya Shamu au kwa Kiingereza Red Sea na kwamba kuanzia wakati wa kutangazwa marufuku hiyo na kuendelea urambazaji wa baharini wa Israel katika Bahari Nyekundu utakuwa shabaha halali ya jeshi la wanajeshi wa Yemen.
-
Jeshi la Iran lashambulia kambi za kimkakati za anga za jeshi la anga la Israel kujibu uchokozi
Jun 08, 2026 11:23Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetangaza kuanzisha “Operesheni Nasr” (Ushindi), likisema limezilenga kambi za kimkakati za anga za utawala wa Israel za Nevatim na Tel Nof, kama hatua ya kujibu mashambulizi ya makombora yaliyolenga vituo vya rada vya Iran.
-
Araghchi afanya mazungumzo ya kidiplomasia kuhusu uchokozi wa Israel
Jun 08, 2026 11:20Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araghchi, amefanya mfululizo wa mazungumzo kwa njia ya simu na baadhi ya mawaziri wenzake wa maeneo mbali mbali duniani pamoja na kamanda wa jeshi, kufuatia hatua ya Iran kujibu ukiukaji wa mara kwa mara wa makubaliano ya usitishaji mapigano nchini Lebanon unaotekelezwa na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Yemen yatangaza marufuku ya meli za Israel katika Bahari ya Sham
Jun 08, 2026 11:13Vikosi vya Jeshi la Yemen vimetangaza marufuku kamili ya usafiri wa baharini wa Israel katika Bahari Nyekundu (Bahari ya Sham), vikisema kwamba harakati zote za adui katika eneo hilo sasa zitachukuliwa kuwa malengo halali ya kijeshi, baada ya kutekeleza shambulizi la kombora lenye usahihi dhidi ya maeneo nyeti ya Israel huko Tel Aviv.
-
Visa vya Ebola vyazidi 500 nchini DRC huku tahadhari ya kuenea zaidi ikitolewa
Jun 08, 2026 11:12Idadi ya visa vilivyothibitishwa vya ugonjwa wa Ebola katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) imefikia 515, vikiwemo vifo 91, huku mamlaka za afya zikionya kuwa maambukizi bado yanaendelea na huenda visa vikazidi kuongezeka ikiwa hatua za udhibiti hazitaimarishwa haraka.
-
Ramaphosa atangaza hatua mpya kukabili uhamiaji haramu Afrika Kusini
Jun 08, 2026 11:10Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa, ametangaza msururu wa hatua mpya zinazolenga kukabiliana na uhamiaji haramu, kufuatia kuongezeka kwa wasiwasi wa umma kuhusu suala hilo.
-
Jibu kali la makombora la Iran kwa ukiukaji wa mara kwa mara wa usitishaji vita na jinai za Israel nchini Lebanon
Jun 08, 2026 08:03Iikiwa ni katika kunufaika na haki yake ya kujilinda na kujibu ukiukaji wa mara kwa mara wa usitishaji vita na jinai za kinyama zinazofanywa na utawala dhalimu wa Israel dhidi ya watu wa Lebanon, vikosi vya jeshi la Iran Jumapili usiku vilitoa jibu kali la makombora katika maeneo ya utawala huo katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu. Maeneo yaliyolengwa katika shambulio hilo kubwa la makombora kimsingi ni ya kijeshi na kistratijia ya utawala wa Israel.
-
Iran yashambulia maeneo yanayokaliwa kwa mabavu, yatahadharisha kuhusu vipigo vikali zaidi' iwapo mashambulizi dhidi ya Lebanon yataendelea
Jun 08, 2026 03:23Vikosi vya ulinzi vya Iran jana usiku viliyatangwa kwa makombora maeneo kadhaa ya Israel, ikiwa ni katika kujibu mashambulizi yanayoendelea ya Israel dhidi ya Lebanon kwa kukiuka makubaliano ya kusitisha mapigano.
-
Iran yasema misimamo ya Marekani “inayobadilika na kinzani” imekwamisha mazungumzo
Jun 08, 2026 03:21Iran imesema mazungumzo yanayoendelea na Marekani bado yamekwama hasa kutokana na misimamo ya Washington inayobadilika mara kwa mara na yenye kauli zinazokinzana. Aidha Marekani inaendelea “kubadilisha vigezo vya mazungumzo.” Hata hivyo, ubadilishanaji wa ujumbe kati ya pande hizo mbili unaendelea kupitia wapatanishi kutoka Pakistan.
-
Kulazimisha Timu ya Taifa ya Iran kuingia na kutoka Marekani siku ya mechi si haki na ni janga
Jun 08, 2026 03:17Kocha wa soka wa Iran na mchezaji wa zamani wa kimataifa ameishutumu serikali ya Marekani kwa kuingiza siasa katika michezo, akitaja vikwazo vya visa na matatizo ya kiutawala yanayowakabili wachezaji na wasimamizi wa Timu ya Taifa ya Soka ya Iran.