-
Iran yasema haitashiriki Kombe la Dunia la FIFA 2026
Mar 12, 2026 06:27Waziri wa Michezo wa Iran, Ahmad Donyamali amesema timu ya taifa ya soka ya Jamhuri ya Kiislamu haitashiriki katika fainali za Kombe la Dunia katika msimu ujao wa joto, licha ya Rais wa Shirikisho la Soka Duniani FIFA, Gianni Infantino kusisitiza kuwa amehakikishiwa na Rais Donald Trump wa Marekani kwamba Iran inakaribishwa kushiriki mashindano hayo makubwa zaidi ya soka duniani, pamoja na vita vinavyoendelea.
-
Korea Kaskazini yampongeza Ayatullah Mojtaba Khamenei kwa kuchaguliwa kuwa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu
Mar 12, 2026 02:50Korea Kaskazini imepongeza Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei kwa kuchaguliwa kwake kuwa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran.
-
Kamanda Hatami: Tutalinda heshima na hadhi ya Iran ya Kiislamu hadi tone la mwisho la damu
Mar 12, 2026 02:27Kamanda Mkuu Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema vijana wa ardhi hii takatifu watalinda heshima ya Iran kwa nguvu na azma hadi tone la mwisho la damu
-
Pezeshkian: Iran haina nia ya kuingia katika mzozo na nchi za eneo
Mar 12, 2026 02:24Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Masoud Pezeshkian, amesisitiza kwamba Iran haitaki vita au uhasama na nchi za eneo, bali inalenga tu vituo vinavyotumiwa kama chanzo cha mashambulizi dhidi ya ardhi yake.
-
Ushiriki wa kihistoria wa wakazi wa Tehran katika mazishi ya Mashahidi wa Vita vya Ramadhani
Mar 11, 2026 13:29Hafla ya mazishi ya Mashahidi wa Vita vya Ramadhani imefanyika kuanzia Uwanja wa Mapinduzi (Maidan-e Enqelab) hadi Mi‘raj al-Shuhadaa jijini Tehran, ikiambatana na mahudhurio makubwa ya wananchi waliokuja kutoa heshima zao za mwisho.
-
Seneta wa Marekani akiri: Hatutafikia malengo yetu yoyote katika vita na Iran
Mar 11, 2026 13:03Chris Murphy, Seneta wa chama cha Democrat nchini Marekani, kufuatia kikao cha faragha na maafisa wa utawala wa Rais Donald Trump kuhusu uvamizi wa kijeshi dhidi ya Iran, amekosoa mtazamo wa utawala huo na kusema: "Hatutafikia malengo yoyote tuliyotangaza katika vita dhidi ya Iran."
-
Seneta wa Marekani akiri: Hatutafikia malengo yetu yoyote katika vita na Iran
Mar 11, 2026 12:43Chris Murphy, Seneta wa chama cha Democrat nchini Marekani, kufuatia kikao cha faragha na maafisa wa utawala wa Rais Donald Trump kuhusu uvamizi wa kijeshi dhidi ya Iran, amekosoa mtazamo wa utawala huo na kusema: "Hatutafikia malengo yoyote tuliyotangaza katika vita dhidi ya Iran."
-
Mufti Mkuu wa Russia ampongeza Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei
Mar 11, 2026 12:08Mufti Mkuu wa Russia ambaye pia ni Mkuu wa Idara ya Masuala ya Kidini ya Waislamu wa Shirikisho la Russia ametuma ujumbe akimpongeza Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei kwa kuchaguliwa kuwa Kiongozi Mpya wa Mapinduzi ya Kiislamu.
-
Iran imeandaa maandamano makubwa ya Siku ya Kimataifa ya Quds
Mar 11, 2026 09:40Maandamano makubwa ya kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Quds yanatarajiwa kufanyika katika miji na maeneo yote ya Iran Ijumaa hii.
-
Mazungumzo ya kikanda kwa ajili ya kufunga kambi za majeshi ya Marekani Asia Magharibi, kisa? Mashambulizi ya Iran
Mar 11, 2026 08:27Duru za kuaminika zimeiambia Rusia Today kwamba nchi za Kiarabu za Ghuba ya Uajemi zimeanza mazungumzo ya kujadili suala la kufunga kwa muda kambi za majeshi ya Marekani katika eneo la Asia Magharibi.