-
Wizara ya Afya ya Kongo: Idadi ya watu wanaoshukiwa kuambukizwa Ebola imepindukia 1,000
May 29, 2026 03:01Wizara ya Afya ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imetangaza kuwa idadi ya watu wanaoshukiwa kuwa na Ebola nchini humo imepindukia 1,000 huku kukiwa na ongezeko la maambukizi katika majimbo ya mashariki mwa nchi hiyo.
-
Washington Post: Israel imetengwa duniani kutokana na vita vya mara kwa mara vya Netanyahu
May 29, 2026 02:57Gazeti la Washington Post limeandika kuwa: Vita vya Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, dhidi ya watu wa Ukanda wa Gaza, Lebanon, Syria, Iran na Yemen vimeiweka Israel katika njia ya mmomonyoko wa kijeshi, kushindwa kimkakati na kutengwa kimataifa.
-
IRGC yasimamia kupita salama meli nyingine 26 katika Mlango wa Hormuz
May 29, 2026 02:54Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limesema meli 26 za kibiashara na meli za mafuta zimevuka Mlango-Bahari wa Hormuz katika muda wa saa 24 zilizopita baada ya kuratibu na kikosi chake cha wanamaji, na kuonya kwamba jaribio lolote la kuvuruga au kifungu njia hiyo ya bahari ya kimkakati litakabiliwa na jibu kali.
-
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu ahimiza kulinda 'neema kubwa' ya umoja wa kitaifa
May 28, 2026 12:46Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema Marekani na Israel, ambazo zimeshindwa katika uvamizi wao wa kijeshi dhidi ya Iran, zinapanga njama ya kupandikiza mzozo na fitina ndani ya Iran.
-
Kundi la kwanza la Waghana lawasili Accra baada ya kurejeshwa kutoka Afrika Kusini
May 28, 2026 11:55Kundi la kwanza la karibu Waghana 300 waliorudishwa kutoka Afrika Kusini kutokana na hujuma za kupinga wahamiaji, liliwasili Accra jana Jumatano.
-
Marekani yarejesha vikwazo dhidi ya Ripota Maalumu wa UN kwa kufichua mauaji ya kimbari ya Israel
May 28, 2026 10:40Marekani imemuwekea tena vikwazo Ripota Maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu maeneo ya Palestina yanayokaliwa kwa mabavu kwa sababu tu ya kufichua mauaji ya kimbari yanayofanywa na utawala wa Israel katika Ukanda wa Gaza.
-
IRGC: Kituo cha uchokozi dhidi ya Bandar Abbas kimelengwa; uchokozi ukirudiwa, jibu litakuwa kali zaidi
May 28, 2026 10:06Idara ya Mahusiano wa Umma ya Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) imetangaza kuwa: Kituo cha anga cha Marekani kilichotumiwa kufanya uchokozi dhidi ya Bandar Abbas kusini mwa Iran, kimelengwa alfajiri ya leo Alkhamisi saa 10:50.
-
Kuanzia "Kujisalimisha Bila Masharti" hadi Kukubali Nguvu ya Iran; Kurudi Nyuma kwa Trump Chini ya Mashinikizo ya Ukweli wa Mambo
May 28, 2026 09:45Kushindwa Trump na Netanyahu katika kufikia malengo yao ya kuishambulia kijeshi Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa mara ya pili katika kipindi cha miezi tisa, ni moja ya mada muhimu zinazojadiliwa na taasisi za utafiti, wananadharia mashuhuri na vyombo tajika vya habari.
-
Wanafunzi 16 wafariki dunia Kenya baada ya moto kuteketeza bweni Utumishi Girls Academy
May 28, 2026 09:39Wanafunzi 16 wameuawa baada ya moto kuteketeza bweni lao usiku wa kuamkia leo katika shule ya bweni huko Gilgil, (Utumishi Girls Academy) yapata kilomita 120 (maili 77) magharibi mwa mji mkuu wa Kenya, Nairobi, mamlaka imethibitisha.
-
IRGC: Iran imepata uwezo mpya wa kukabiliana na maadui
May 28, 2026 04:49Afisa mmoja mwandamizi wa kijeshi ameonya kwamba uchokozi wowote mpya wa kijeshi dhidi ya Iran utasababisha jibu la aina tofauti na lenye nguvu zaidi, “lisilofanana na chochote walichowahi kukiona hapo kabla.”