IRGC yasimamia kupita salama meli nyingine 26 katika Mlango wa Hormuz
-
Meli na boti ya kijeshi ya IRGC
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limesema meli 26 za kibiashara na meli za mafuta zimevuka Mlango-Bahari wa Hormuz katika muda wa saa 24 zilizopita baada ya kuratibu na kikosi chake cha wanamaji, na kuonya kwamba jaribio lolote la kuvuruga au kifungu njia hiyo ya bahari ya kimkakati litakabiliwa na jibu kali.
Ofisi ya Uhusiano wa Umma ya Jeshi la Wanamaji la IRGC jana ilieleza kuwa jeshi hilo linasimamia kwa busara" mlango bahari huo kwa "mamlaka kamili," na kusisitiza kuwa meli zote zinapasa kupata kibali na kuwasiliana na kikosi cha wanamaji kabla ya kuvuka ukanda huo muhimu.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, meli kadhaa zilijaribu kuingia kinyume cha sheria katika Ghuba ya Uajemi baada ya kuzima mifumo yao ya ufuatiliaji baharini, na kuchukuliwa hatua na IRGC.
"Jumatano usiku, meli kadhaa zilijaribu kuingia katika Ghuba ya Uajemi kinyume cha sheria. Kikosi cha Wanamaji cha IRGC kilisimamisha meli mbili kati hizo katika Mlango Bahari wa Hormuz, na meli nyingine mbili zililazimika kurudi nyuma." Imeeleza taarifa ya IRGC.