Mar 27, 2024 07:38
Jeshi katili la Israel limeendelea kuushambulia kwa mabomu mji wa Rafah wa kusini mwa Ukanda wa Gaza, licha ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kupasisha azimio la kusimamisha vita huko Gaza baada ya miezi sita ya mashambulizi ya jeshi la utawala huo wa Kizayuni katika eneo hilo.