Dec 23, 2023 08:18
Ijumaa ya jana, Desemba 22, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilipitisha azimio la kuongeza misaada ya kibinadamu kwa watu wa Ukanda wa Gaza bila kutoa wito wa kusitishwa mapigano. Marekani na Russia, wanachama wawili wa kudumu wa Baraza la Usalama, hazikulipigia kura azimio hilo. Wajumbe wengine 13 wamelipigia kura ya ndiyo.