Watu karibu 30 wameuawa na wengine zaidi ya 50 kujeruhiwa katika mapigano mapya yaliyozuka kati ya vikosi vya majimbo mawili hasimu yenye mamlaka ya ndani nchini Somalia.
Watu 18 wameuawa na wengine zaidi ya 20 wamejeruhiwa katika mapigano makali kati ya wakulima na wafugaji nchini Niger.
Habari kutoka Bangui, mji mkuu wa Jamhuri ya Afrika ya Kati zinaarifu kuwa, watu zaidi ya 11 wameuawa huku wengine 14 wakitoweka kufuatia mapigano makali yaliyojiri baada ya kuuawa mwanajeshi wa nchi hiyo ya kati kati mwa Afrika.
Watu 10 wameuawa katika mapigano kati ya pande zilizosaini makubaliano ya amani huko Mali.
Msemaji wa kiongozi wa upinzani nchini Sudan Kusini amesema Riek Machar ameikimbia nchi hiyo kutokana na kuandamwa na maafisa usalama wa serikali, ambao wamekuwa wakimsaka kwa udi na uvumba tangu aukimbie mji mkuu Juba zaidi ya mwezi mmoja uliopita.
Kwa akali watu watatu wameuawa katika wimbi jipya la mashambulizi ya makundi ya waasi katika Jamhuri ya Afrika ya Kati.
Wafuasi wa karibu wa Riek Machar, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Sudan Kusini wamedai kuwa Rais Salva Kiir anapanga njama ya kujaza nafasi ya Machar ambaye kwa sasa hayuko katika mji mkuu Juba.
Watu kadhaa wameuawa na kujeruhiwa katika mapigano ya kikabila yaliyojiri katika kijiji kimoja mkoani Kivu ya Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Makamu wa Rais wa Sudan Kusini Riek Machar ameondoka katika mji mkuu wa nchi hiyo Juba pamoja na askari wanaomuunga mkono na kwenda kusikojulikana.
Baada ya siku moja ya mapigano ya umwagaji damu kati ya waungaji mkono na wapinzani wa Sudan Kusini katika mji mkuu Juba, kumeripotiwa kutokea ufyatualianaji risasi katika eneo lililopo jirani na ikulu ya Rais.