Makumi ya watu wameuawa na wengine wengi kujeruhiwa katika shambulizi la kigaidi lililolenga msikiti wa Kishia katika mji mkuu wa Afghanistan, Kabul, wakati wa maadhimisho ya Arubaini ya Imam Hussein AS.
Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imelaani shambulio la kigaidi lililotokea jana Jumamosi katika mkoa wa Baluchestan nchini Pakistan, ambapo makumi ya watu waliuawa na wengine wengi kujeruhiwa.
Kundi moja la kigaidi na kitakfiri nchini Afghanistan limefanya shambulizi la pili dhidi ya Waislamu wa madhebu ya Shia waliokuwa wamekusanyika msikitini wakifanya maombelezo ya kukumbuka kuuawa shahidi Imam Hussein AS.
Makumi ya watu wameuawa na kujeruhiwa katika shambulizi la bomu la kutegwa garini lililolenga wanajeshi wa serikali katika mji wa Benghazi, mashariki mwa Libya.
Kwa akali watu 10 wameuawa katika mashambulizi pacha ya mabomu ya kutegwa garini katika makao makuu ya Idara ya Upelelezi mjini Mogadishu nchini Somalia.
Makumi ya wanachama wa kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh wameuawa katika operesheni kali ya jeshi la Afghanistan, katika mkoa wa Nangarhar, kaskzini mwa nchi.
Mashambulizi pacha ya mabomu yamesababisha vifo vya watu zaidi ya 13 karibu na kambi ya Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Afrika nchini Somalia AMISOM na nje ya ofisi za Umoja wa Mataifa katika mji mkuu Mogadishu.
Rais Francois Hollande wa Ufaransa amesema serikali yake itatafanya kila liwezekanalo ili kukomesha kikamilifu mashambulizi na harakati za kundi la kigaidi na kitakfiri la Desh (ISIS) nchini humo.
Mbunge wa zamani katika Kongresi ya Marekani amefichua nafasi ya utawala wa kizayuni wa Israel katika mashambulizi ya kigaidi yanayofanyika barani Ulaya.
Kwa akali watu 18 wameuawa na wengine 23 kujeruhiwa katika hujuma nyingine ya kigaidi mashariki mwa Iraq, siku moja baada ya shambulizi jingine la bomu kuua na kujeruhi makumi ya watu katika mji mkuu Baghdad.