-
UNHCR: Hali ya wakimbizi Sudan Kusini ni mbaya sana
Jul 12, 2016 12:32Shirika la Wakimbizi la Umoja wa Mataifa (UNHCR) limetangaza kuwa hali ya raia wanaokimbia vita na mapigano ya ndani Sudan Kusini inatia wasiwasi mkubwa.
-
Pande hasimu nchini Sudan Kusini zatangaza usitishaji vita
Jul 12, 2016 03:17Pande mbili zinazohasimiana huko Sudan Kusini na kusababisha kuzuka upya kwa vurugu nchini humo zimetangaza kusitishwa kwa mapigano, baada ya kuwepo kwa siku kadhaa za machafuko mjini Juba zilizosababisha vifo vya mamia ya watu.
-
Raia wa Uganda wazuiwa kutembelea Sudan Kusini
Jul 11, 2016 23:16Jeshi la polisi la Uganda jana liliwapiga marufuku raia wa nchi hiyo kutembelea Sudan Kusini baada ya kuzuka mapigano mapya katika mji mkuu wa nchi hiyo Juba na kupelekea watu wasiopungua 300 kuuawa.
-
Kikao cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu Sudan Kusini
Jul 11, 2016 08:28Wanachama 15 wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa wametoa taarifa wakitaka kuhitimishwa mapigano katika mji mkuu wa Sudan Kusini, Juba.
-
Uganda haitatuma UPDF S/Kusini huku KQ ikisimamisha safari za ndege Juba
Jul 11, 2016 02:57Jeshi la Ulinzi la Uganda UPDF limesema halitatuma askari wake kwenda kudhibiti hali ya mambo nchini Sudan Kusini, muda mfupi baada ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuzitaka nchi za kanda ya Afrika Mashariki kuingilia kati na kusuluhisha mgogoro na mapigano mapya yaliyozuka nchini humo.
-
Umoja wa Mataifa watiwa wasiwasi na mapigano yanayoendelea Sudan Kusini
Jul 09, 2016 11:31Mapigano yaliyoshtadi katika siku kadhaa zilizopita huko Sudan Kusini yamemfanya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kueleza wasiwasi wake kutokana na machafuko yanayoendelea huko Juba mji mkuu wa nchi hiyo.
-
Wanajeshi 115 wauawa katika mapigano Juba, Sudan Kusini
Jul 09, 2016 10:26Wanajeshi wasiopungua 115 wameuawa Sudan Kusini katika mapignao baina ya mirengo hasimu serikalini katika mji mjuu Juba.
-
Mapigano yaendelea kushuhudiwa Sudan Kusini
Jul 09, 2016 03:10Baada ya siku moja ya mapigano ya umwagaji damu kati ya waungaji mkono na wapinzani wa Sudan Kusini katika mji mkuu Juba, kumeripotiwa kutokea ufyatualianaji risasi katika eneo lililopo jirani na ikulu ya Rais.
-
Uganda, Sudan Kusini kupambana na wizi wa mifugo
Jul 04, 2016 03:22Serikali za Uganda na Sudan Kusini zimeafikiana kupambana na wizi wa mifugo na haswa ng'ombe unaofanyika mara kwa mara katika vijiji vilivyoko mpakani mwa nchi mbili hizo.
-
Wakazi wa Magharibi mwa Sudan Kusini wakimbia mapigano
Jul 03, 2016 23:36Shirika la Madaktari Wasio na Mipaka limeripoti kuwa wakazi wa eneo moja huko magharibi mwa Sudan Kusini wameyakimbia makazi yao kufuatia kujiri mapigano ya silaha kati ya jeshi la Sudan Kusini na makundi yenye silaha.