Makumi ya watu wameuawa katika wimbi jipya la mapigano kati ya askari wa jeshi la serikali na waasi katika mji wa Wau nchini Sudan Kusini.
Mkuu wa mkoa wa mashariki mwa Jamhuri ya Afrika ya Kati ametangaza kuwa waasi wa kundi la Lord's Resistance Army (LRA) kutoka Uganda wameteka nyara watu 17 na kuwapeleka kusikojulikana.
Uganda imesema karibuni hivi itawaondoa askari wake wanaoongoza katika operesheni ya kuwasaka waasi wa Lord's Resistance Army (LRA) katika Jamhuri ya Afrika ya Kati.
Hali imeendelea kuwa tete nchini Burundi licha ya Rais Pierre Nkurunzinza kutoa muda maalumu kwa kundi la wapinzani wa serikali, wa kuachana na upinzani wao.
Kamanda mmoja wa jeshi la Uganda amesema kuwa, hali ya usalama imesharejea kaskazini mwa nchi hiyo, na ndio maana sheria ya hali ya hatari imeondolewa.
Afisa mmoja mwandanamizi wa jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ametangaza habari ya kutiwa mbaroni waasi kadhaa wa kundi la Mai Mai, mashariki mwa nchi hiyo.
Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo limeanzisha opereseheni mpya ya kijeshi dhidi ya waasi wa Uganda, mashariki mwa nchi hiyo.
Rais Paul Kagame wa Rwanda amekanusha nchi yake kuwasaidia waasi wa Burundi kama ilivyokuja katika ripoti ya siri iliyowasilishwa kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
Ofisi ya uratibu wa misaada ya kibinadamu ya Umoja wa Mataifa imesema kuwa, hali mbaya na machafuko huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ni kikwazo kikuu cha kuwafikishia misaada ya kibinadamu wahitaji.
Kundi la waasi la Lord's Resistance Army la Uganda liliwateka watu 296 katika Jamuhuri ya Afrika ya Kati na Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo katika robo ya kwanza ya mwaka huu.