-
Akademia ya Geneva: Waliofariki Ghaza wanakaribia 200,000, watu wamepungua kwa 10%
Feb 08, 2026 02:26Stuart Casey Maslen, mkuu wa Akademia ya Geneva ya Sheria za Kimataifa za Kibinadamu na Haki za Binadamu amesema, tangu Oktoba 2023 hadi sasa, idadi ya watu huko Ghaza imepungua kwa zaidi ya 10%, hali inayoashiria kutokea vifo takribani laki mbili.
-
Hali yazidi kuwa mbaya Gaza: Uhaba wa dawa na vifaa vya matibabu washadidi
Feb 07, 2026 12:09Wizara ya Afya ya Palestina katika Ukanda wa Gaza imetangaza katika taarifa yake kwamba, hospitali zilizobaki zinazofanya kazi katika Ukanda huo, ambazo zinajitahidi kuendelea kutoa huduma za kimatibabu, zimekuwa vituo vya kusubiri maelfu ya wagonjwa na majeruhi ambao wanakabiliwa na hatima isiyojulikana.
-
Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi lakaribisha mazungumzo ya Iran na Marekani
Feb 07, 2026 11:55Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi limetangaza kuwa, limekaribisha kwa mikono miwili mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja kati ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Marekani yaliyofanyika Muscat Oman.
-
Zaidi ya wagonjwa 11,000 wa saratani Ukanda wa Gaza wanakabiliwa na kifo
Feb 07, 2026 02:45Mkurugenzi wa Taasisi ya Haki za Binadamu ya Al-Dameer amekosoa vikali utaratibu wa sasa wa kivuko cha Rafah, akikiita "tasa na hatari" na kuonya kwamba utaratibu wa sasa umesababisha ongezeko lisilotarajiwa la idadi ya vifo miongoni mwa wagonjwa wa saratani katika Ukanda wa Gaza.
-
Olmert akiri: Maangamizi ya kizazi cha Wapalestina yanafanyika Ukingo wa Magharibi
Feb 06, 2026 10:10Waziri Mkuu wa zamani wa utawala wa kizayuni wa Israel Ehud Olmert amekiri kwamba polisi, jeshi na Shirika la Usalama wa Ndani la utawala huo (Shabak) wanahusika katika mashambulizi yaliyopangwa na walowezi dhidi ya Wapalestina katika Ukingo wa Magharibi, akielezea vitendo hivyo kama njama ya kijinai na utumiaji nguvu ya uangamizaji wa kizazi cha Wapalestina.
-
Euro-Med Monitor: EU ni mshiriki wa mauaji ya kimbari Gaza
Feb 06, 2026 06:23Shirika la kutetea haki za binadamu la Euro-Mediteranean Human Rights Monitor (Euro-Med Monitor) lenye makao yake makuu huko Geneva, Uswisi limekosoa vikali msimamo wa Umoja wa Ulaya kwa kuweka masharti yasiyotekelezeka kwa ajili ya ujenzi mpya wa Gaza.
-
Hamas yalaani mashambulizi ya Israel Ukanda wa Gaza; Netanyahu amekusudia kukwamisha mapatano
Feb 06, 2026 02:30Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) imelaani mashambulizi makubwa ya anga ya Israel katika Ukanda wa Gaza yaliyouwa shahidi Wapalestina 23 tangu ustishaji vita wa Oktoba mwaka jana na ksuema kuwa hujuma hiyo ya utawala wa Kizayuni inathibitisha kuwa namna Israel inavyoendeleza kampeni yake ya mauaji ya kimbari.
-
Human Rights Watch: Israel inafanya mauaji ya halaiki Ukanda wa Gaza
Feb 05, 2026 11:39Shirika la Kutetea Haki za Binadamu la Human Rights Watch limetangaza kuwa, utawala wa Israel unafanya mauaji ya halaiki katika Ukanda wa Gaza, Palestina.
-
Guardiola apaza sauti tena kuhusu mauaji ya kimbari ya Ghaza na dhulma inayotawala duniani
Feb 05, 2026 06:05Kocha wa timu ya soka ya Manchester City, Pep Guardiola, amesema mauaji ya watu wasio na hatia duniani kote yanamuathiri sana na amewahimiza walimwengu wasinyamazie kimya dhulma zinazofanywa.
-
Vita vya kieneo; maana yake na jinsi vinavyotokea
Feb 05, 2026 02:32Kwa mujibu wa ripoti ya Pars Today, kutokana na uchochezi na vitisho vya mara kwa mara vya Marekani dhidi ya Iran, Tehran imeonya kwamba shambulio lolote la kijeshi kutoka Marekani dhidi ya Iran litasababisha kuwashwa moto wa vita vya eneo. Sasa swali linaibuka: vita vya eneo ni nini na vinafanyika vipi?