-
Israel imeficha gharama za vita
Mar 17, 2025 08:16Vyombo vya habari vya Israel vimeripoti kuwa gharama za vita za utawala huo zimefichwa mwaka huu, tofauti na ripoti za mwaka jana, na kuna wasiwasi kuhusu usimamizi wa bajeti.
-
Hamas: Vitisho vya Marekani vinatatiza zaidi hali ya mambo
Mar 17, 2025 08:13Msemaji wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) amesisitiza kuwa: Vitisho vya Marekani vinapelekea tu hali ya mambo kuwa ngumu zaidi.
-
Vikosi vya Ulinzi vya Yemen vyaishambulia kwa mara ya pili manowari ya kubebea ndege za kivita ya US
Mar 17, 2025 02:08Vikosi vya Ulinzi vya Yemen vimeishambulia kwa mara ya pili manowari ya kubebea ndege za kivita ya Marekani ya USS Harry Truman na kuzima mashambulizi ya anga yaliyokuwa yamedhamiriwa kufanywa na Washington dhidi ya nchi hiyo.
-
UNICEF: Asilimia 90 ya wakazi wa Ghaza wanashindwa kupata maji safi ya kunywa
Mar 17, 2025 02:07Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) limetahadharisha kuwa uhaba mkubwa wa maji katika Ukanda wa Ghaza umefikia hatua mbaya na ya maafa, kwa ababu karibu asilimia 90 ya wakazi wa eneo hilo wanashindwa kupata maji safi ya kunywa.
-
Hizbullah: Lebanon haitaanzisha katu uhusiano wa kidiplomasia na utawala wa Kizayuni Israel
Mar 17, 2025 02:06Mwakilishi wa Hizbullah katika Bunge la Lebanon amesisitizia msimamo wa kudumu wa nchi hiyo kuhusiana na utawala wa Kizayuni wa Israel na akasema, Lebanon kamwe haitokubali kufuata mkondo wa kuanzisha uhusiano wa kidiplomasia na utawala huo ghasibu.
-
Hamas yalaani ya mashambulizi ya Marekani na Uingereza dhidi ya Yemen
Mar 16, 2025 23:07Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imelaani vikali mashambulizi ya anga ya Marekani na Uingereza dhidi ya maeneo ya makazi ya watu huko Sana'a, mji mkuu wa Yemen.
-
Yemen: Tutatoa jibu la 'kitaalamu na chungu' kwa shambulio baya la Marekani
Mar 16, 2025 08:13Baraza Kuu la Kisiasa la Yemen limelaani shambulio baya la Marekani dhidi ya nchi hiyo kwa kuunga mkono Israel, na kuapa kuwa taifa hilo la Kiarabu litauadhibu utawala huo wa kihalifu kwa njia "ya uchungu".
-
Israel imeua zaidi ya Wapalestina 150 tangu usitishaji vita ulipoanza kutekelezwa Ghaza Januari 19
Mar 16, 2025 07:22Ofisi ya Vyombo vya Habari ya Serikali ya Palestina katika Ukanda wa Ghaza imetangaza kuwa, zaidi ya Wapalestina 150 wameuliwa shahidi na jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel- tangu makubaliano ya kusitisha mapigano yalipoanza kutekelezwa katika eneo hilo Januari 19 mwaka huu-, wakiwemo 40 waliouawa katika kipindi cha wiki mbili zilizopita.
-
Makundi ya Muqawama yalaani vikali jinai mpya za Marekani nchini Yemen
Mar 16, 2025 02:35Harakati mbalimbali za Muqawama zimelaani vikali kwa kauli moja jinai zinazoendelea kufanywa na Marekani na Uingereza dhidi ya Yemen, katika njama za Washington na London za kujaribu kuulinda utawala ghasibu wa Israel mbele ya operesheni za Sana’a zinazofanyika kama sehemu ya kuliunga mkono taifa madhlumu la Palestina.
-
Duru za Wazayuni: Hamas inajijenga upya kwa kasi kubwa
Mar 16, 2025 02:35Chombo komoja cha habari cha lugha ya Kiebrania kimezinukuu duru za usalama na kijasusi za Israel zikidai kuwa, kasi ya kujijenga upya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palesitna HAMAS kwa siku moja ni sawa na utendaji wa Israel kwa mwezi mzima.