Seneta wa Marekani: Vikwazo vyetu dhidi ya Iran, Russia na China havina tija yoyote
Seneta Rand Paul wa chama cha Republican nchini Marekani amesema sera ya Washington ya kuendelea kushadidisha vikwazo dhidi ya Russia, China na Iran haina tija yoyote.
Katika hotuba yake hiyo, Seneta huyo amesema, amekuwa akiuliza mara kwa mara suali lifuatalo kwa maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje: "hivi mnaweza kuniambia kama kuna mwenendo mmoja tu ambao umebadilika kutokana na vikwazo? Niambieni kama kuna kikwazo kimoja mlichoiwekea Russia kikaifanya Russia iseme: 'tunaomba radhi kwa hilo, haikutupasa kamwe kufanya hivyo. Na tutafanya kile hasa mnachotaka tufanye, tuambieni tu nini cha kufanya na tutafanya.' Au niambieni kama kuna mwenendo mmoja tu ambao umebadilishwa na China, au na Russia au na Iran. Kwa kweli ukiitazama Iran ni kinyume chake hasa".