Maandamano London ya kupinga kuuziwa silaha Riyadh
https://parstoday.ir/sw/news/world-i39947-maandamano_london_ya_kupinga_kuuziwa_silaha_riyadh
Makumi ya watu juzi waliandamana na kukusanyika mbele ya ubalozi wa Saudi Arabia mjini London Uingereza wakipinga na kulalamikia hatua ya Uingereza ya kuiuzia silaha Saudia.
(last modified 2023-11-27T08:44:11+00:00 )
Feb 05, 2018 04:23 UTC
  • Maandamano London ya kupinga kuuziwa silaha Riyadh

Makumi ya watu juzi waliandamana na kukusanyika mbele ya ubalozi wa Saudi Arabia mjini London Uingereza wakipinga na kulalamikia hatua ya Uingereza ya kuiuzia silaha Saudia.

Wafanya maandamano hayo wamelalamikia na kukosoa hatua ya Uingereza ya kuendelea kuiuzia silaha Saudi Arabia ambayo inaongoza muungano vamizi katika kuishambulia Yemen. Ian Pocock Msemaji wa harakati kwa jina la Campaign Against Arms Trade (CAAT) amesema kuwa serikali ya Uingereza imeuuzia utawala wa Saudia silaha zenye thamani ya pauni bilioni moja na milioni mia sita tangu mwezi Machi mwaka 2015; na kwamba  silaha hizo hadi sasa zimeuwa maelfu ya raia wa Yemen na kuisababishia nchi hiyo maafa na hasara mbalimbali. 

Maafa ya mashambulio ya Saudia dhidi ya makazi ya raia huko Yemen 
 

Msemaji wa Kampeni dhidi ya Biashara ya Silaha  ameongeza kuwa serikali ya Uingereza inapasa kuhitimisha hatua yake ya kuiuzia Riyadh silaha na kwamba ni wazi kuwa London inahusika katika kuvamiwa kijeshi Yemen. Wakati huo huo Ian Pocock amewatolea wito wananchi wa Uingereza kulalamikia  hatua ya nchi yao ya kuiuzia Saudi Arabia silaha kwa ajili ya kuzitumia dhidi ya wananchi wa Yemen.