Assalaam Aleikum wapenzi wasikilizaji wa Idhaa ya Kiswahili, Sauti ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inayokutangazieni kutoka mjini Tehran, na karibuni kusikiliza sehemu nyingine ya kipindi hiki cha Ruwaza Njema. Kipindi hiki kama mnavyojua huzungumzia Hadithi tofauti kutoka kwa watu wa Nyumba ya Mtume Mtukufu (saw) ambazo hutuongoza na kutuwezesha kuiga tabia njema za mtukufu huyo katika maisha yetu ya kila siku.