-
WHO: Yumkini ugonjwa hatari wa Ebola umesambaa hadi nchini Rwanda
Jul 18, 2019 07:31Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema mwanamke raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo aliyeaga dunia mapema mwezi huu kutokana na homa hatari ya Ebola aliingia nchini Rwanda akiwa ameathiriwa na ugonjwa huo na huenda alisambaza virusi hivyo nchini humo kabla ya kuelekea nchini Uganda alikofia.
-
WHO yatahadharisha kuhusu hatari ya kuenea homa ya Ebola huko Kongo DR
Jul 17, 2019 07:58Shirika la Afya Duniani (WHO) limetahadharisha kuwa mlipuko wa homa ya Ebola ulioukumba mji wa Goma mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo huwenda ukawa na athari mbaya sana.
-
UN: Kunahitajika mamilioni ya dola kwa ajili ya kupambana na Ebola, DRC
Jul 15, 2019 07:02Mkuu wa masuala ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa, mlipuko wa ugonjwa wa Ebola huko katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo huwenda ukaendelea kuwepo kwa kipindi kirefu, kuua idadi zaidi ya watu na kugharibu fedha nyingi iwapo nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa hazitatoa mamia ya mamilioni ya dola kwa sasa kwa ajili ya kupambana na kasi ya ugonjwa huo.
-
Mgonjwa mwenye dalili za Ebola Kenya awekwa karantini
Jun 17, 2019 08:01Mgonjwa anayeshukiwa kuwa na Ebola nchini Kenya amewekwa katika karantini katika Hospitali ya Kericho magharibi mwa nchi hiyo.
-
Mtu wa pili afariki dunia kwa Ebola Uganda, mijumuiko hadharani marufuku Kasese
Jun 13, 2019 07:21Uganda imepiga marufuku mijumuiko hadharani katika Wilaya ya Kasese baada ya ugonjwa hatari wa Ebola kuibuka katika eneo hilo.
-
Ebola yaua katika kesi ya kwanza ya ugonjwa huo nchini Uganda
Jun 12, 2019 08:28Kijana aliyekuwa na umri wa miaka mitano ameaga dunia kutokana na ugonjwa wa Ebola, hii ikiwa ni kesi ya kwanza ya maradhi hayo hatari kuthibitishwa katika nchi hiyo ya Afrika Mashariki.
-
Kesi nyingine elfu moja za Ebola zagunduliwa DRC
Jun 09, 2019 22:06Hujuma na mashambulizi dhidi ya makundi ya madaktari Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ni kikwazo kikubwa cha kupambana na ugonjwa hatari wa Ebola nchini humo.
-
Jeshi la DRC laua wanamgambo 26 katika mji ulioathiriwa na Ebola
May 30, 2019 21:58Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo limetangaza habari ya kuua wanamgambo 26 karibu na mji wa Beni ulioathiriwa na ugonjwa hatari wa Ebola, mashariki mwa nchi.
-
Tishio la ugonjwa wa Ebola kuenea kote Afrika Mashariki
May 26, 2019 03:07Jumuiya ya Afrika Mashariki EAC imetahadahrisha kuhusu tishio la ugonjwa hatari wa Ebola kuenea katika nchi za jumuiya hiyo.
-
Mapigano katika mji ulioathiriwa na Ebola DRC yaua watu 9
May 08, 2019 09:15Kwa akali watu tisa wameripotiwa kupoteza maisha katika mapigano baina ya askari wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na wanamgambo waliobeba silaha katika mji wa Butembo ulioathiriwa na ugonjwa hatari wa Ebola.