-
The Guardian: Imarati imempatia Haftari tani 5,000 za silaha
Mar 13, 2020 02:50Ripoti iliyoandikwa na gazeti la Guardian la Uingereza imefichua kuwa, nchi ya Umoja wa Falme wa Kiarabu (Imarati) imempatia jenerali mstaafu wa Libya, Khalifa Haftar tani elfu tano za silaha tangu mwezi Januari mwaka huu.
-
Waziri wa zamani wa Algeria kuwa mjumbe maalumu wa UN nchini Libya
Mar 12, 2020 07:56Waziri wa zamani wa mambo ya nje wa Algeria ametangazwa kuwa chaguo la baadae la kushika nafasi ya mjumbe wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya Libya.
-
Kuendelea mashauriano kwa ajili ya kurejesha hali ya uthabiti Libya
Mar 11, 2020 07:08Katika hali ambayo vita vinaendelea huko Libya; Khalifa Haftar kamanda wa wanamgambo kwa jina la jeshi la kitaifa la Libya ameainisha masharti kwa ajili ya kutekeleza usitishaji vita huko Libya wakati alipokutana na kufanya mazungumzo na Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa katika ikulu ya Elysee.
-
UNICEF: Vita nchini Libya vimekuwa na taathira mbaya mno hasa kwa watoto
Mar 05, 2020 08:18Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa (UNICEF) umetangaza kuwa, watu wasiopungua 1,800,000 wameathirika vibaya na vita vya ndani nchini humo ambapo 266,000 kati yao ni watoto wadogo.
-
Mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya Libya ajiuzulu
Mar 03, 2020 07:25Ghassan Salamé, mjumbe maalumu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya Libya ametangaza kujiuzulu wadhifa huo, huku mgogoro wa nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika ukishtadi.
-
Indhari ya UN kuhusu kubadilika mzozo wa Libya kuwa vita vya kieneo
Mar 02, 2020 00:20Licha ya mazungumzo na juhudi za kimataifa katika wiki za hivi karibuni kwa ajili ya kuhitimisha vita nchini Libya, lakini mapigano yamezidi kuongezeka na sasa nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika imegeuka kuwa ulingo wa vita vya niaba.
-
UN: Mapigano ya ndani Libya yanaweza kugeuka kuwa vita vya kieneo
Feb 29, 2020 07:13Mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Libya ametahadharisha kuwa mapigano ya ndani nchini humo yanaweza kugeuka kuwa vita vya kieneo.
-
Al-Sarraj ailaumu Jumuiya ya Nchi za Kiarabu kwa kushindwa kuutatua mgogoro wa Libya
Feb 26, 2020 12:44Kiongozi wa Serikali ya Maafikiano ya Kitaifa ya Libya (GNA) ameilaumu Jumuiya ya Nchi za Kiarabu kwa kushindwa kutatua mgogoro wa nchi hiyo.
-
Imarati yawatumia wapiganaji wa Haftar ndege 100 zilizosheheni silaha
Feb 25, 2020 08:00Imebainika kuwa, ndege 100 za mizigo zilizosheheni silaha na zana za kijeshi zimewasili nchini Libya zikitokea Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati).
-
Waziri Mkuu wa Libya: Haftar ni mtenda jinai za kivita
Feb 25, 2020 01:22Fayez al Serraj Waziri Mkuu wa serikali ya umoja wa kitaifa ya Libya amelaani kushambuliwa maeneo ya raia na viwanja vya ndege nchini humo kunakofanywa na wanamgambo wanaoongozwa na Jenerali Khalifa Haftar.