-
Wapinzani DRC watoa sharti la kukubali muafaka wa kisiasa
Dec 24, 2016 04:15Wapinzani katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wametoa sharti ambalo wanasema lazima upande wa serikali ulikubali ili waunge mkono muafaka hafifu wa kisiasa uliofikiwa jana.
-
Mgogoro wa kisiasa Kongo DR wapatiwa ufumbuzi?
Dec 23, 2016 12:54Katika hatua ya ghafla na ambayo haikutazamiwa na wengi, pande hasimu za kisiasa katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo zimefikia muafaka, ambao utapelekea Rais Joseph Kabila asalie uongozini hadi mwishoni mwa mwaka ujao 2017.
-
Iran na Kyrgyzstan zasaini hati tano za mapatano ya ushirikiano
Dec 23, 2016 03:25Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran leo Ijumaa amekutana na Rais Almazbek Atambayev wa Kyrgyzstan katika ikulu ya rais huyo mjini Bishkek na kufanya mazungumzo kuhusu kuimarisha uhusiano wa pande pamoja na masuala mbalimbali ya kieneo na kimataifa.
-
Assad: Kukombolewa Aleppo ni ushindi kwa Syria, Iran na Russia
Dec 22, 2016 11:15Rais Bashar al-Assad wa Syria amesema kukombolewa kikamilifu mji wa kistratejia wa Aleppo (Halab), kaskazini magharibi mwa nchi ni ushindi mkubwa sio tu kwa taifa hilo, bali pia kwa Iran na Russia.
-
Muhula wa Rais Kabila DRC wamalizika, serikali yazima mitandao ya kijamii
Dec 16, 2016 04:49Katika hali ambayo muhula wa kisheria wa kuwa uongozini Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo unaelekea kumalizika, serikali ya Kinshasa imeagiza kukatwa mawasiliano kwenye mitandao ya kijamii.
-
Rais wa Sudan Kusini ataka kufanyika Mazungumzo ya Kitaifa
Dec 15, 2016 00:49Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini ametoa wito wa kufanyika 'Mazungumzo ya Kitaifa' ili kuupatia ufumbuzi mzozo wa kisiasa na kiusalama unaoikabili nchi hiyo.
-
Rais Rouhani amlaki rasmi Rais wa Indonesia
Dec 14, 2016 04:45Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amemlaki rasmi Rais wa Indonesia katika Ikulu ya Saad Abad hapa Tehran.
-
Kiongozi wa upinzani ashinda uchaguzi wa rais Ghana, Mahama akubali matokeo
Dec 10, 2016 04:04Kiongozi mkongwe wa upinzani nchini Ghana, Nana Akufo-Addo, ameibuka mshindi katika uchaguzi wa rais uliofanyika Jumatano iliyopita na kumshinda Rais wa sasa John Dramani Mahama.
-
Rais wa Ghana: Upinzani unawashawishi wafuasi wake wasikubali matokeo ya uchaguzi
Dec 07, 2016 00:28Rais John Dramani Mahama wa Ghana amemtuhumu kiongozi mkuu wa upinzani nchini humo kuwa anawashawishi wafuasi wa chama chake wasikubali matokeo ya uchaguzi wa Rais na Bunge unaofanyika leo nchini humo.
-
Mkulima wa ndizi ashinda uchaguzi wa rais nchini Haiti
Nov 29, 2016 09:46Jovenel Moise, mkulima wa ndizi na mfanyabiashara mashuhuri ameibuka mshindi katika uchaguzi wa rais nchini Haiti.