-
13 wauawa katika mashambulizi pacha ya mabomu Mogadishu, Somalia
Jul 26, 2016 16:54Mashambulizi pacha ya mabomu yamesababisha vifo vya watu zaidi ya 13 karibu na kambi ya Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Afrika nchini Somalia AMISOM na nje ya ofisi za Umoja wa Mataifa katika mji mkuu Mogadishu.
-
Watu kadhaa wauawa katika machafuko mapya CAR
Jul 25, 2016 08:08Kwa akali watu watatu wameuawa katika wimbi jipya la mashambulizi ya makundi ya waasi katika Jamhuri ya Afrika ya Kati.
-
Mauaji ya Waislamu wa Srebrenica yakumbukwa
Jul 11, 2016 16:59Maelfu ya watu leo wameshiriki katika shughuli ya kukumbuka maelfu ya Waislamu wa Srebrenica waliouawa kinyama na Waserbia wa Bosnia Herzegovina miaka kadhaa iliyopita.
-
Al-shabaab washambulia kambi ya jeshi na kuua askari 10
Jul 11, 2016 07:49Kundi la kigaidi na kitakfiri la al-Shabaab limeshambulia kwa bomu kambi moja ya jeshi kusini magharibi mwa mji mkuu wa Somalia Mogadishu na kuua wanajeshi 10 wa nchi hiyo ya Pembe ya Afrika.
-
Polisi 4 wa Marekani wauawa Dallas, maelfu wapinga ukatili wa polisi
Jul 08, 2016 08:20Maafisa 4 polisi ya Marekani wameuwa baada ya 11 miongoni mwao kupigwa risasi katika maandamano ya wananchi wanaopinga ukatili wa polisi ya nchi hiyo dhidi ya Wamarekani weusi katika mji wa Dallas, Texas.
-
Askari 12 wa Libya wauawa katika hujuma ya bomu Benghazi
Jul 07, 2016 14:06Kwa akali askari 12 wa jeshi la Libya wameuawa katika shambulizi la bomu la kutegwa garini katika mji wa Benghazi, mashariki mwa nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika.
-
Waasi wa ADF waua watu 9 kaskazini mwa Kongo DR
Jul 06, 2016 04:31Watu 9 wameuawa na kundi la waasi wa ADF-Nalu wa Uganda kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
-
80 wauawa katika mashambulizi ya mabomu Baghdad, Iraq
Jul 03, 2016 07:22Watu wasiopungua 80 wameuawa na wengine wengi kujeruhiwa katika mashambulizi pacha ya mabomu katika mji mkuu wa Iraq, Baghdad.
-
Askari 6 wa Misri wauawa katika mpaka na Libya
Jul 01, 2016 08:04Habari kutoka Cairo, mji mkuu wa Misri zinasema kuwa, kwa akali skari 6 wa jeshi la nchi hiyo wameuawa kwenye makabiliano na kundi la watu wanaofanya magendo ya silaha na mihadarati katika mpaka wa nchi hiyo na Libya.
-
18 waua katika shambulizi la bomu nchini Somalia
Jun 30, 2016 08:16Kwa akali watu 18 wameripotiwa kuuawa na wengine wengi kujeruhiwa katika shambulizi la bomu mapema leo katika mji wa Lafole, kusini magharibi mwa Somalia.