Wapinzani wakusanyika Kisangani wakitaka kuachiwa huru wafungwa wa kisiasa
https://parstoday.ir/sw/news/africa-i17146-wapinzani_wakusanyika_kisangani_wakitaka_kuachiwa_huru_wafungwa_wa_kisiasa
Wapinzani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wamekusanyika katika mji wa Kisangani nchini humo wakitaka kuachiwa huru wanaharakati wa kisiasa wanaoipinga serikali.
(last modified 2023-11-27T08:44:11+00:00 )
Oct 10, 2016 10:44 UTC
  • Wapinzani wakusanyika  Kisangani wakitaka kuachiwa huru wafungwa wa kisiasa

Wapinzani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wamekusanyika katika mji wa Kisangani nchini humo wakitaka kuachiwa huru wanaharakati wa kisiasa wanaoipinga serikali.

Benjamin Ntumba mmoja wa wanaharakati wa chama cha Upinzani cha  Umoja kwa ajili ya Demokrasia na Maendeleo ya Jamii (UDPS) amesema kuwa wapinzani Kongo  wamekusanyika katika mji wa Kisangani kulalamikia hatua ya Mahakama moja mjini humo ya kukataa kuwaachia huru wapinzani sita wa kisiasa.

Benjamin Ntumba mwanaharakati wa chama cha upinzani Kongo cha (UDPS)

Wanaharakati hao sita wa kisiasa wanaoipinga serikali ya Kinshasa wanashikiliwa mahabusu huko Kisangani tangu tarehe 19 mwezi uliopita hadi sasa. Benjamin Ntumba ameashiria  kuachiwa huru watu wengine ambao walitiwa mbaroni pamoja na wanaharakati hao sita na kusisitiza kuwa, wanaharakati hao wa kisiasa wanaoipinga serikali ya Kongo wamekatwa kinyume cha sheria. Ntumba ametaka wanaharakati hao waachiwe huru haraka na bila ya masharti yoyote.