-
Azma thabiti ya Iran na Pakistan ya kuimarisha uhusiano na ushirikiano wa kupambana na ugaidi
Jan 19, 2024 23:30Baada ya kushadidi mivutano ya mpakani kati ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Pakistan katika kipindi cha siku mbili zilizopita, viongozi wa Tehran na Islamabad wamesisitiza kuendeleza uhusiano wa kirafiki kati ya nchi mbili, kuheshimiwa umoja wa ardhi za mataifa hayo mawili na kuwepo uratibu na mashauriano ya karibu zaidi katika kupambana na magenge ya kigaidi.
-
Mitazamo inayokinzana ya utawala wa Biden kuhusu Ansarullah ya Yemen
Jan 19, 2024 07:08Sera na mienendo ya hivi karibuni ya serikali ya Joe Biden kuhusu harakati ya Ansarullah ya Yemen inaonyesha kusanganyikiwa kwa serikali ya Washington
-
Indhari ya Uhispania kuhusu matukio ya eneo na ya kimataifa ya vita vya Gaza
Jan 18, 2024 23:57Pedro Sánchez, Waziri Mkuu wa Uhispania ameonya kuwa, usalama na uthabiti wa eneo la Asia Magharibi (Mashariki ya Kati) umekuwa hatarini na kwamba, mashambulizi haya yanahatarisha nidhamu na uratibu wa ushirikiano wa pande kadhaa.
-
Himaya mpya ya Magharibi kwa Israel
Jan 18, 2024 05:05Wakati ambapo utawala wa Kizayuni wa Israel bado unaendeleza mauaji yake dhidi ya Wapalestina wa Gaza, nchi za Magharibi nazo zinaendelea kutoa himaya na misaada kwa utawala huo, na kinyume na madai yote ya eti kutetea haki za kibinadamu yanayotolewa na nchi hizo, zinaiwezesha Israel kuendeleza vita vya mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina.
-
Umuhimu wa uchaguzi katika mustakbali wa nchi na kushindwa njama za maadui wa Iran ya Kiislamu
Jan 17, 2024 08:01Uchaguzi wa awamu ya kumi na mbili ya Majlisi ya Ushauri wa Kiislamu ya Iran (Bunge) na awamu ya sita ya Wanazuoni Wataalamu wa Kumchagua Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi utafanyika tarehe Pili Marchi mwaka huu nchini Iran katika huku hali ya ndani na ya kimataifa ikizidisha maradufu umuhimu na udharura wake.
-
Operesheni kabambe ya Iran ya kujibu jinai za magenge ya kigaidi katika eneo na waungaji mkono wao wa Magharibi
Jan 17, 2024 04:02Vikosi vya Ulinzi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran vimeshambulia kwa mpigo kupitia operesheni mbili tofauti makao makuu ya magenge ya kigaidi katika nchi za Iraq na Syria, likiwa ni jibu kwa vitendo vya magenge hayo na kwa moto wa vita unaoendelea kukolezwa na utawala haramu wa Kizayuni na waungaji mkono wake wa Magharibi.
-
Sababu za vita vya Gaza kuendelea kwa muda mrefu
Jan 17, 2024 01:03Licha ya kupita siku 100 tangu vita vya utawala wa Kizayuni dhidi ya Ukanda wa Gaza vianze, lakini bado hakuna matarajio ya kumalizika kwa vita hivyo.
-
Kuongezeka uwepo kijeshi wa Marekani huko Iraq na Syria
Jan 16, 2024 10:57Marekani ilituma wanajeshi huko Iraq mwaka 2003 wakati ilipoivamia na kuikalia kwa mabavu nchi hiyo mwaka 2003; na kuhusu Syria pia Marekani ilituma wanajeshi wake nchini humo mwaka 2014 kwa kisingizio cha kupambana na kundi la kigaidi la Kitakfiri la Daesh (ISIS) katika fremu ya Muungano wa Kimataifa wa eti kukabiliana na ugaidi.
-
Kushtadi mipasuko ya ndani katika utawala wa Kizayuni wa Israel
Jan 16, 2024 03:02Katika hali ambayo, zimepita siku 100 tangu kuanza vita vya utawala wa Kizayuni dhidi ya Ukanda wa Gaza, vita hivyo vinaonekana kushadidisha migawanyiko na mipasuko ya ndani katika ardhi hizo zinazokaliwa kwa mabavu (Israel).
-
Kuongezeka hitilafu katika serikali ya Biden kuhusiana na vita vya Gaza
Jan 15, 2024 23:15Sambamba na uendelea vita vya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya watu madhulumu wa Ukanda wa Gaza huko Palestina, kuzidi kuzorota hali ya mambo katika eneo la Magharibi mwa Asia na himaya ya wazi na ya siri ya Marekani kwa utawala huo ghasibu, ushahidi uliopo unaonyesha kuwa hali inazidi kuwa ngumu kwa Marekani siku baada ya siku kutokana na kuendelea kuunga mkono jinai za Israel, hasa mauaji ya halaiki ya Wapalestina.