Rais Pezeshkian: Iran inalenga kuimarisha uhusiano na Oman
https://parstoday.ir/sw/news/iran-i133360-rais_pezeshkian_iran_inalenga_kuimarisha_uhusiano_na_oman
Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesifu uhusiano imara kati ya Iran na Oman, na kueleza kuwa Tehran ina imani kwamba uhusiano wa pande mbili utaendelea kukua kwa "nguvu na uthabiti.
(last modified 2025-11-19T06:59:18+00:00 )
Nov 19, 2025 06:59 UTC
  • Rais Pezeshkian: Iran inalenga kuimarisha uhusiano na Oman

Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesifu uhusiano imara kati ya Iran na Oman, na kueleza kuwa Tehran ina imani kwamba uhusiano wa pande mbili utaendelea kukua kwa "nguvu na uthabiti.

Rais Pezeshkian alisema jana wakati wa kupokea hati za utambulisho za Sayyid Yaarub bin Qahtan bin Nasser Albusaidi, Balozi mpya wa Oman nchini Iran kwamba , kuna kiwango cha juu cha "maelewano, uhusiano, na ushirikiano kati ya  Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Oman. 

Amesema nchi mbili zinatilia mkazo haja ya kuimarisha na kupanua zaidi ushirikiano huu kuliko hapo awali. 

Rais Masoud Pezeshkian ameashiria ziara yake ya karibuni huko Muscat mji mkuu wa Oman na kusema makubaliano muhimu na yenye manufaa yalifikiwa kati ya nchi mbili akiwa ziarani nchini humo. 

Amesema nchi mbili zimejitolea kutekeleza makubaliano haya na kuyafuatilia.  

Kwa upande wake, Albusaidi amesema "Sultan wa Oman anasisitiza sana kudumisha uhusiano imara na nchi rafikina ndugu ya Iran Iran  amani, utulivu na ustawi.