-
Rais wa Iran yuko Oman kujadili njia za kukomesha jinai za Israel Gaza
May 27, 2025 08:31Dkt. Masoud Pezeshkian, Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, kabla ya kuanza ziara yake rasmi ya siku mbili nchini Oman, ameeleza kuwa lengo kuu la safari hiyo ni kufanya mashauriano ya kina kwa ajili ya kukomesha uhalifu wa utawala wa Kizayuni, sambamba na kuimarisha mahusiano ya pande mbili katika nyanja mbalimbali.
-
Iran yaambia Marekani: Urutubishaji madini ya urani 'hauwezi kujadiliwa'
May 27, 2025 08:27Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kwamba taifa la Iran halitikisiki mbele ya mbinu za mashinikizo za Marekani, na kutupilia mbali madai ya Washington yanayotaka Jamhuri ya Kiislamu iachane na haki yake halali ya kutumia nishati ya nyuklia kwa malengo ya amani.
-
Mtaalamu wa UN: Dunia iilazimishe Israel kusitisha mauaji ya kimbari Gaza
May 27, 2025 08:15Mtaalamu maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu katika maeneo ya Palestina yanayokaliwa kwa mabavu amekemea vikali Israel kwa kuwachoma hai watu, hasa watoto, katika Ukanda wa Gaza, ambako utawala huo unaendesha vita vya mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina.
-
Je, Iran na nchi za Afrika zinawezaje kukamilishana kiuchumi?
May 27, 2025 07:31Sayyid Abbas Araghchi, Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Iran amesema kuwa serikali ya Iran inalipa kipaumbele maalumu suala la mahusiano na bara la Afrika, na ameonesha matumaini ya mustakabali mwema katika ushirikiano wa pande mbili.
-
Pezeshkian: Iran inaunga mkono usitishaji vita baina ya India-Pakistan
May 27, 2025 03:09Rais Masoud Pezeshkian wa Iran kwa mara nyingine tena amesisitiza kuwa, Jamhuri ya Kiislamu inaunga mkono usitishaji vita wa kudumu kati ya India na Pakistan, akitoa mwito wa kufanyika mazungumzo kati ya nchi za kikanda ili kutatua mizozo iliyopo na kuimarisha amani.
-
Kiongozi Muadhamu: Hatua madhubuti zinahitajika kukomesha jinai za Ghaza
May 26, 2025 23:26Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitizia ulazima wa kuweko hatua za pamoja na zenye ufanisi baina ya Iran na Pakistan za kukomesha jinai za utawala wa Kizayuni huko Ghaza na ameashiria nafasi maalumu ya Pakistan katika ulimwengu wa Kiislamu.
-
Baqhaei: Iran haitaki kupoteza muda katika mazungumzo
May 26, 2025 06:53Msemaji huyo wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema: Tatizo kubwa zaidi katika eneo letu hili litabakia kuwa ni kuendelea mauaji ya umati huko Palestina mauaji ambayo yanaumiza moyo wa kila mtu aliye huru, na huwezi kuzungumzia mambo yanayoendelea katika eneo hili na kunyamazia kimya jinai za utawala wa Kizayuni. Aidha amesema, Iran haitaki kupoteza muda kwenye mazungumzo.
-
Araghchi: Iran ina azma ya kuimarisha ushirikiano wa kiuchumi na Afrika
May 26, 2025 03:49Abbas Araghchi, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, amesema kuwa serikali ya Iran chini ya uongozi wa Rais Masoud Pezeshkian inalipa kipaumbele maalum suala la mahusiano na bara la Afrika, na ameonesha matumaini ya mustakabali mwema katika ushirikiano wa pande mbili. Amesema kuwa Iran inatafuta fursa za ushirikiano wa kiuchumi na nchi za Afrika katika muktadha wa Eneo Huru la Biashara la Bara la Afrika (AfCFTA)
-
Araghchi "Ufaransa Haina Mamlaka ya Kimaadili ya Kuihubiria Iran"
May 26, 2025 02:52Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amelaani vikali matamshi ya hivi karibuni ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Ufaransa, Jean-Noel Barrot, aliyoyataja kuwa ya chuki dhidi ya Iran.
-
Kamanda wa IRGC: Iran kwenye vita kamili, lakini nchi iko katika utulivu
May 25, 2025 08:04Kamanda Mkuu wa Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amesema: Tuko kwenye vita kamili, lakini hakuna chochote kinachoonekana kuwa katika hali ya vita; medani za mapambano ziko hai, lakini nchi iko katika hali ya utulivu.