-
Russia: Wamagharibi wakubali haki ya Iran ya kurutubisha madini ya urani na waache lugha ya vitisho
Nov 22, 2025 03:47Serikali ya Russia imeyataka madola ya Magharibi kuachana na lugha ya vitisho na badala yake yatambue na kuikubali haki ya Iran ya kurutuubisha madini ya urani.
-
Moscow: Stratijia ya Magharibi ya mashinikizo na vikwazo dhidi ya Iran haina tija
Nov 21, 2025 23:51Mjumbe wa Baraza la Uhusiano Baina ya Kaumu Mbalimbali linalosimamiwa na Rais Vladimir Putin wa Russia amesema vikwazo vya nchi za Magharibi dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran havitafua dafu.
-
Haj Ali Akbari: Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki hauna thamani yoyote kwa watu wa Iran
Nov 21, 2025 07:51Khatibu wa Swala ya Ijumaa ya leo mjini Tehran amekosoa mashirika ya kimataifa kwa hatua zao zisizo na maana na zisizoaminika, akisema: "Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki (IAEA) halina thamani yoyote kwa taifa la Iran."
-
Araghchi: Iran imejiandaa zaidi kukabiliana na uhasama wa Israel
Nov 21, 2025 04:31Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, amesema kuwa Jamhuri ya Kiislamu sasa imejiandaa kuliko wakati wowote kukabiliana na uhasama wowote kutoka Israel.
-
Azimio jipya la Bodi ya Magavana ya IAEA lina lengo la kufidia kushindwa Marekani na Troika ya Ulaya
Nov 20, 2025 23:33Mwakilishi wa kudumu na balozi wa Iran katika taasisi za kimataifa zenye makao yake mjini Vienna Austria amesema kupitishwa azimio la kisiasa dhidi ya nishati ya nyuklia ya Iran yenye malengo ya amani ni jaribio la Marekani na Umoja wa Ulaya ili kufidia kushindwa kwao katika utaratibu wa Snapback huko New York.
-
Kharrazi amwambia Trump: Huwezi kuilazimisha Iran kufumbia macho haki zake
Nov 20, 2025 06:47Kamal Kharrazi, mshauri wa ngazi za juu wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei ametoa ujumbe wa wazi kwa Marekani na kusema kuwa, siasa za Donald Trump za kutumia mabavu haziwezi kuifanya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kubadilisha njia yake.
-
Iran yalaani shambulio la kigaidi la Israel na Marekani dhidi ya wakimbizi ya Palestina Lebanon
Nov 20, 2025 06:46Iran imelaani vikali shambulio la hivi karibuni la kigaidi lililofanywa na Israel kwa msaada kamili wa Marekani dhidi ya kambi kubwa zaidi ya wakimbizi ya Palestina kusini mwa Lebanon ikisema kwamba Marekani inahusika moja kwa moja na jinai hiyo.
-
Araghchi: Hatutakubali kwa namna yoyote ile kushusha urutubishaji urani hadi kiwango cha sifuri
Nov 20, 2025 03:23Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Sayyid Abbas Araghchi amesema: "hatutakubali kwa namna yoyote ile kushusha urutubishaji wa urani hadi kiwango cha sifuri kwa sababu hili limekuwa ni jambo la fakhari na heshima kwa taifa, tumetumia gharama nyingi sana za kimaada na kimaanawi kwa ajili yake, na tumepoteza wanasayansi kadhaa waliouawa shahidi kwa ajili ya kulidumisha".
-
Iran: Azimio la Marekani lililopasishwa na UN kuhusu Gaza linahalalisha ukaliaji mabavu
Nov 19, 2025 09:16Iran imekosoa azimio lililoandaliwa na Marekani na kupasishwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa linaloweka utaratibu wa kutumwa Gaza usimamizi wa nchi ajinabi na kutahadharisha kuwa azimio hilo linadhoofisha haki za msingi za watu wa Palestina.
-
Grossi: Wakaguzi wa wakala wa IAEA wamerejea Iran
Nov 19, 2025 08:35Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) amesema katika kikao cha robo mwaka cha Bodi ya Magavana ya wakala huo kwamba: "Wakaguzi wa IAEA wamerejea Iran na wamefanya ukaguzi katika vituo ambavyo havikuathiriwa na mashambulizi ya Juni, lakini ushirikishwaji zaidi unahitajika ili kurejesha ukaguzi kamili."