-
Tamko la Marekani baada ya Mahakama ya Kenya kusitisha ujenzi wa kituo cha Ebola
May 30, 2026 11:32Mahakama Kuu ya Kenya imesitisha kwa muda kuanzishwa kituo cha karantini kwa wagonjwa wa Ebola raia wa Marekani, kilichotarajiwa kujengwa nchini humo. Kufuatia uamuzi huo, wakuu wa Marekani wamedai kuwa watashughulikia hofu ya Wakenya kuhusiana na kituo hicho.
-
Iran yasema mapatano na Marekani bado hayajafikiwa, yakataa mabavu ya Trump
May 30, 2026 11:01Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema Ijumaa kwamba mabadilishano ya ujumbe kati ya Iran na yanaendelea, lakini hadi sasa hakuna mwafaka wa mwisho uliofikiwa huku akisisitiza kuwa Tehran haikubali lugha ya mabavu.
-
Mshauri wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu aonya: Trump anaisaliti diplomasia kwa mara ya tatu
May 30, 2026 10:59Mshauri mwandamizi wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu ameonya kuwa Rais wa Marekani Donald Trump anaisaliti diplomasia na kuupa nafasi mwelekeo wa vita kwa mara ya tatu, kutokana na kile alichokitaja kuwa ni hatua zake za kichokozi.
-
UN: Asilimia 100 ya Gaza ni mali ya Wapalestina, yataka Israel ikomeshe uvamizi haramu
May 30, 2026 10:29Umoja wa Mataifa umekosoa vikali mipango ya Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, ya kupanua udhibiti juu ya Ukanda wa Gaza, na kusisitiza kuwa eneo lote ni haki ya watu wa Palestina.
-
Almasi Zilizochongwa kwa Machozi ya Afrika-Sehemu ya Kwanza: Maumivu ya Ukoloni
May 30, 2026 08:17Wapenzi wasikilizaji, Ukoloni wa karne ya kumi na tisa haukuwa wa kuhodhi ardhi tu za mataifa, bali ulikuwa mfumo na utaratibu maalumu ulioratibiwa kwa ajili ya kuuhamisha utajiri wa Afrika na kuupeleka Ulaya. Katika kipindi kilichojulikana kama “ Uvamizi wa Afrika”, Uingereza ilitumia nguvu zake za kiuchumi pamoja na makampuni binafsi kuanzisha ubeberu wa kimuundo na ulio endelevu wa kuzihodhi rasilimali za bara hilo.
-
Kwa nini utawala wa Kizayuni unasisitiza kuendeleza vita huko Lebanon?
May 30, 2026 07:00Moja ya vikwazo muhimu katika mazungumzo ya Iran na Marekani ni sisitizo la utawala wa Kizayuni wa Israel la kuondolewa medani ya vita vya Lebanon kwenye mazungumzo hayo na kuendeleza vita dhidi ya harakati ya Hizbullah. Hii ni katika hali ambayo Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetangaza kuwa moja ya masharti muhimu ya kufikiwa mapatano na Marekani ni kusimamishwa kikamilifu vita katika ngome zote za mhimili wa muqawama na hasa nchini Lebanon.
-
Iran yakemea vikali tishio la Marekani la kuiwekea Oman vikwazo
May 30, 2026 04:50Iran yakemea vikali tishio la Marekani la kuiwekea Oman vikwazo
-
Mahakama Kuu ya Katiba ya Madagascar yapinga kuondolewa madarakani Rais
May 30, 2026 04:13Mahakama Kuu ya Katiba ya Madagascar imepinga jaribio la mbunge wa upinzani la kumwondoa madarakani Rais Michael Randrianirina wa nchi hiyo.
-
WHO yakadiria kiwango cha vifo vya Ebola kufikia asilimia 30-50 wakati mkuu wake akizuru DRC
May 30, 2026 03:34Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema kuwa kiwango cha vifo katika mripuko wa sasa wa ugonjwa wa Ebola nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) ni kati ya asilimia 30 na 50, huku mkuu wa shirika hilo akizuru nchi hiyo kusaidia juhudi za kuudhibiti ugonjwa huo hatari.
-
Hizbullah: Hakuna njia nyingine isipokuwa mapambano dhidi ya Israel
May 30, 2026 03:27Mbunge mwandamizi wa Lebanon amesema kuwa harakati ya Hizbullah itaendeleza operesheni zake za kijeshi dhidi ya vikosi vya utawala dhalimu wa Israel.