-
Majeshi ya majini ya Iran, Afrika Kusini na Sri Lanka kushirikiana usalama baharini
Feb 20, 2026 03:45Kamanda wa Jeshi la Wanamaji wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza udharura wa ushirikiano kati ya vikosi vya majini vya Iran na vile vya Afrika Kusini na Sri Lanka ili kukabiliana na vitisho vya pamoja na kuhakikisha usalama endelevu katika maji ya kimataifa.
-
Mauzo ya nje ya kilimo ya Iran yaongezeka, asilimia 85 ya chakula ni uzalishaji wa ndani
Feb 20, 2026 03:44Waziri wa Jihadi ya Kilimo wa Iran ametangaza ongezeko kubwa la mauzo ya nje ya kilimo hapa nchini hadi dola bilioni nane na kutangaza kwamba asilimia 85 ya usalama wa chakula wa Iran inadhaminiwa na uzalishaji wa ndani.
-
Russia yakanusha madai ya kuwaajiri Wakenya katika vita vya Ukraine
Feb 20, 2026 03:42Russia imekanusha madai kwamba inawaajiri Wakenya kupigana vitani nchini Ukraine, kufuatia ripoti za Huduma ya Kijasusi ya Kitaifa ya Kenya kwamba zaidi ya Wakenya 1,000 kwa sasa wanapigana upande wa Russia katika mzozo huo.
-
Zaidi ya Wapalestina na Waarabu 9,300 wanashikiliwa mateka katika magereza ya Israel
Feb 20, 2026 03:41Klabu ya Wafungwa wa Palestina imetangaza kuwa, zaidi ya mateka na wafungwa 9,300 wa Palestina na Kiarabu wanashikiliwa katika magereza ya utawala ghasibu wa Israel na wamekuwa wakikabiliwa na sera za mateso, njaa, na mauaji ya taratibu tangu kuanza "mauaji ya kimbari ya Israel" mnamo Oktoba 7, 2023.
-
Nchi 30, Tume ya EU yatoa wito wa kukomeshwa mara moja mapigano Sudan
Feb 20, 2026 03:41Wawakilishi kutoka nchi 30 na Tume ya Umoja wa Ulaya wametoa wito wa kukomeshwa mara moja uhasama nchini Sudan, wakielezea wasiwasi mkubwa kuhusu kuendelea mashambulizi ya mauti dhidi ya raia kote nchini humo.
-
Kiongozi Muadhamu ahudhuria hafla ya Qur'ani siku ya kwanza ya Ramadhani
Feb 19, 2026 23:58Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Seyyed Ali Khamenei amehudhuria kikao cha kiroho cha Qur'ani katika siku ya kwanza ya mwezi mtukufu wa Ramadhani, akijumuika na maqarii na wasomaji mashuhuri wa Iran na kimataifa wa Qur'ani Tukufu.
-
Wachunguzi wa UN: Yumkini mauaji ya halaiki yamefanyika El-Fasher
Feb 19, 2026 23:57Ujumbe wa kutafuta ukweli wa Umoja wa Mataifa umesema ukatili uliofanywa na Vikosi vya Usaidizi wa Haraka RSF wakati wa kuutwaa mji wa El-Fasher huko Darfur Magharibi nchini Sudan mwezi Oktoba mwaka jana, una "alama za mauaji ya kimbari" dhidi ya jamii za Zaghawa na Fur.
-
Magaidi wa Lakurawa waua watu 34 kaskazini mwa Nigeria
Feb 19, 2026 23:57Kwa akali watu 34 wameuawa katika mashambulizi ya wanamgambo wa Lakurawa kwenye vijiji kadhaa katika jimbo la Kebbi, kaskazini magharibi mwa Nigeria, ripoti ya usalama iliyoonekana na Reuters ilisema Alkhamisi.
-
Rais wa zamani wa Korea Kusini afungwa maisha jela
Feb 19, 2026 23:56Mahakama ya Korea Kusini jana Alkhamisi ilimhukumu rais wa zamani wa nchi hiyo, Yoon Suk Yeol kifungo cha maisha jela kwa kutangaza sheria ya kijeshi mnamo Desemba 2024, na kumtia hatiani mwanasiasa huyo mwenye umri wa miaka 65 kwa kuongoza uasi na kuhujumu katiba.
-
Waholanzi 640 waliohudumu katika jeshi la Israel Gaza kushtakiwa?
Feb 19, 2026 23:56Zaidi ya raia 640 wa Uholanzi wamehudumu katika jeshi la Israel wakati wa vita vya mauaji ya halaiki vya utawala huo wa Kizayuni dhidi ya Gaza na kwneye mashambulizi dhidi ya Ukingo wa Magharibi, takwimu mpya zinaonyesha, huku wataalamu wa sheria wakionya kwamba, wale waliohusika wanaweza kushtakiwa chini ya sheria za kimataifa na za nchi hiyo za uhalifu wa kivita.