-
Sheikh Qassem: Hizbullah haina lengo la kuanzisha vita, lakini kamwe haitasalimu amri
Feb 17, 2026 03:37Sheikh Naim Qassim Katibu Mkuu wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa harakati hiyo ya muqawama haitaki vita lakini imejiandaa kikamilifu kuilinda Lebanon na kutoa jibu kali kwa uchokozi wowote wa maadui wa nchi hiyo.
-
Mawakili wa Morocco wahitimisha mgomo wao baada ya serikali kuunga mkono muswada wa marekebisho
Feb 17, 2026 03:33Mawakili nchini Morocco wamehitimisha mgomo wa wiki moja baada ya serikali kusimamisha muswada wa kudhibiti sekta ya sheria na kuunda tume iliyopewa jukumu la kuanzisha mazungumzo.
-
Wakenya: Mradi wa kilimo wa Israel Nakuru ni mwanzo wa unyakuzi wa ardhi zetu
Feb 17, 2026 02:52Mradi wa Israel wa kilimo na makazi wa ekari 520 huko Solai, Kaunti ya Nakuru nchini Kenya umezua mjadala mkali wa kitaifa. Wakenya wametumia mitandao ya kijamii kupinga mradi huo, wanaotaja kuwa mwanzo wa unyakuzi wa ardhi za nchi hiyo na utawala ghasibu wa Israel.
-
Kikosi cha Majini cha IRGC chafanya luteka Ghuba ya Uajemi, Hormuz
Feb 16, 2026 23:28Kamanda wa Kikosi cha Wanamaji cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amesisitiza kwa mara nyingine tena kwamba, Iran inadumisha ufuatiliaji kamili wa kijasusi wa saa 24 katika Lango-Bahari la Hormuz.
-
Iran: Tumeingia katika mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja na Marekani kwa nia njema
Feb 16, 2026 23:05Ismail Baqaei Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa Tehran imeingia katika mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja na Marekani kwa mtazamo wenye mwelekeo wa matokeo, huku ikibainisha shaka kuhusu taarifa zinazokinzana za Washington.
-
Idadi ya waliofariki dunia kutokana na kimbunga nchini Madagascar imefikia 59
Feb 16, 2026 22:58Idara yaMaafa ya Majanga ya Kimaumbile ya Madagascar imetangaza kuwa hadi sasa watu 59 wamefariki dunia kutokana na kimbunga cha Gezani kilichoathiri maeneo ya pwani ya mashariki mwa nchi hiyo tarehe 10 mwezi huu huku watu 15 hawajulikani walipo. Wakati huo huo watu zaidi ya 16,000 wamepoteza makazi yao kufuatia kimbunga hicho.
-
Watu 3 wameuawa na 7 kujeruhiwa katika shambulio la droni la RSF hospitalini katika jimbo la Sennar, Sudan
Feb 16, 2026 22:57Mashambulizi wa ndege zisizo na rubani (droni) ya wanamgambo wa Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF)yameuwa watu watatu na kuwajeruhi wengine saba katika Hospitali ya Al-Mazmoum katika jimbo la Sennar kusini mashariki mwa Sudan.
-
Waziri Mkuu wa Ethiopia: Hatuna nia ya kujitanua ili kuifikia bahari
Feb 16, 2026 22:56Waziri Mkuu wa Ethiopia jana alisema kuwa nchi yake "haina nia ya kujitanua" na haina lengo la kuwatishia majirani zake. Amesema vipaumbele muhimu vya kitaifa ni kufikia njia ya baharini na maendeleo ya maji ya Mto Nile.
-
Mijibizo dhidi ya njama za Israel za kuendeleza uporaji na ukaliaji wa mabavu wa ardhi za Ukingo wa Magharibi
Feb 16, 2026 22:54Makundi ya Wapalestina na nchi kadhaa za eneo zimetoa mjibizo kwa mpango wa utawala wa Kizayuni wa Israel wa kuvamia na kuyakalia kwa mabavu maeneo kadhaa ya ardhi za Ukingo wa Magharibi, zikisisitiza kwamba, huo ni ukiukaji wa wazi wa sheria za kimataifa.
-
Araghchi, Grossi wakutana Geneva kabla ya mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja na US
Feb 16, 2026 08:20Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Nishati ya Atomiki (IAEA), Rafael Grossi wamekutana katika jiji la Geneva nchini Uswisi, kabla ya mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja na Marekani.