-
Iran yasisitiza kuwa itavishambulia vituo vya kijeshi vya Marekani, si ardhi za nchi jirani
Feb 08, 2026 02:49Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Sayyid Abbas Araghchi ameonya kwamba, iwapo Marekani itaishambulia Iran, vituo vya kijeshi vya nchi hiyo katika eneo la Asia Magharibi navyo vitashambuliwa.
-
Gaidi aliyefunzwa na Mossad kuendesha 'vita vya mitaani' aangamizwa na vikosi vya intelijensia vya Iran
Feb 08, 2026 02:49Sadeq Ashtari, kiongozi wa genge la kigaidi aliyepewa mafunzo na shirika la ujasusi la utawala wa kizayuni wa Israel Mossad kwa ajili ya kuendesha "vita vya mitaani" ameangamizwa katika mapigano na vikosi vya intelijensia vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Italia yasema haiwezi kujiunga na 'Bodi ya Amani' ya Trump, sababu ni kukinzana na katiba yake
Feb 08, 2026 02:48Italia imesema haiwezi kujiunga na kinachoitwa "Bodi ya Amani" ya Rais wa Marekani Donald Trump kutokana na "mpaka wa kikatiba" ukiwa ni mkwamo mpya na wa karibuni zaidi kukikabili "chombo hicho cha kimataifa cha kujenga amani", alichojibunia rais wa Marekani.
-
Katibu Mkuu wa UN alaani vikali kushadidi machafuko Sudan Kusini, ataka mapigano yasitishwe
Feb 08, 2026 02:47Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amelaani vikali kushadidi kwa machafuko na mapigano nchini Sudan Kusini, ambako watu wapatao milioni 10, wakiwa ni zaidi ya theluthi mbili ya idadi ya watu wote nchini humo, wanahitaji msaada wa kibinadamu wa kuokoa maisha na wanaendelea kuathirika zaidi na mgogoro huo.
-
Maelfu ya Wairaqi wajiandikisha kuingia vitani kuisaidia Iran endapo itashambuliwa na Marekani
Feb 08, 2026 02:46Maelfu ya Wairaqi wamesaini hati ya ahadi ya kusaidia kuihami Jamhuri ya Kiislamu ya Iran iwapo itashambuliwa kijeshi na Marekani.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran: Hatutafanya mazungumzo kuhusu makombora yetu, si sasa wala baadaye
Feb 07, 2026 23:18Sayyid Abbas Araghchi, Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, amesisitiza kwamba Iran haitafanya mazungumzo kuhusu makombora yake, kwa sababu maudhui hiyo inahusu masuala ya ulinzi tu.
-
Tanzania, Uganda kuanza kuuza mafuta ghafi Julai mwaka huu
Feb 07, 2026 23:18Rais Samia Suluhu Hassan wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amesema mafuta ghafi yatakayopita katika Mradi wa Bomba la Mafuta (EACOP) kutoka Hoima, Uganda hadi Tanga, Tanzania yataanza kusafirishwa kwenda sokoni ifikapo Julai, mwaka huu.
-
Waziri wa Fedha wa US akiri hadharani: Tulisababisha uhaba wa dola ndani ya Iran ili kuchochea machafuko
Feb 07, 2026 23:00Waziri wa Fedha wa Marekani Scott Kenneth Homer Bessent amekiri kuwa, Washington ilisababisha uhaba wa sarafu ya dola ya nchi hiyo ndani ya Iran, hatua ambayo ilisababisha kushuka kwa kasi kwa thamani ya sarafu ya Iran ya riali na kuibua mashinikizo ya kiuchumi yaliyochochea machafuko ya Desemba mwaka jana.
-
Shambulio la droni la RSF laua watu 24 wakiwemo watoto 8 Kordofan Kaskazini, Sudan
Feb 07, 2026 22:59Shambulio la ndege zisizo na rubani la Vikosi vya Usaidizi wa Haraka RSF lililolenga gari lililobeba familia za raia wa Sudan waliolazimika kuyahama makazi yao limeua watu wasiopungua 24, wakiwemo watoto wanane. Hayo ni kwa mujibu wa shirika la mtandao wa Madaktari wa Sudan.
-
Akademia ya Geneva: Waliofariki Ghaza wanakaribia 200,000, watu wamepungua kwa 10%
Feb 07, 2026 22:56Stuart Casey Maslen, mkuu wa Akademia ya Geneva ya Sheria za Kimataifa za Kibinadamu na Haki za Binadamu amesema, tangu Oktoba 2023 hadi sasa, idadi ya watu huko Ghaza imepungua kwa zaidi ya 10%, hali inayoashiria kutokea vifo takribani laki mbili.