-
Wafuasi wa Imam Mahdi wakusanyika Jamkaran kuonesha imani na tumaini siku ya Nisf Sha’ban
Feb 04, 2026 10:36Maelfu ya waumini na wafuasi wa Imam Mahdi (Mwenyezi Mungu Aharakishe Kudhihiri Kwake) wamekusanyika katika Msikiti mtukufu wa Jamkaran, mjini Qom, katika siku tukufu za mwezi wa Sha’ban, na kugeuza eneo hilo kuwa ishara yenye nguvu ya imani, mshikamano, na matarajio yenye matumaini kwa mustakabali.
-
Jalali: Madai ya Trump kwamba anawaunga mkono Wairani hayana msingi
Feb 04, 2026 07:25Balozi wa Iran nchini Russia, Kazem Jalali amepuuzilia mbali matamshi ya hivi karibuni ya Rais wa Marekani Donald Trump akidai kuwa analiunga mkono na kulisaidia taifa la Iran, akisisitiza kuwa madai hayo hayana msingi wowote.
-
Seneta wa Nigeria: Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran, nembo ya uhuru duniani
Feb 04, 2026 06:54Seneta Shehu Sani wa Nigeria ambaye pia ni mkuu wa Jukwaa la Haki za Kiraia la Nigeria (CRCN), amesema Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran ya mwaka 1979 ni vuguvugu la mwamko wa kihistoria dhidi ya dhulma na ubeberu wa maajinabi, akiyaelezea mapinduzi hayo kama kigezo cha mataifa yanayokandamizwa duniani kote.
-
Israel yaendelea kumwaga damu za Wapalestina, yaua 20 Gaza
Feb 04, 2026 06:53Mashambulizi mapya ya kinyama ya utawala wa Kizayuni wa Israel yamewaua shahidi watu wasiopungua 20, wakiwemo watoto wadogo katika Ukanda wa Gaza.
-
ANC yamkosoa Mfalme wa Afrika Kusini kwa kuwaalika maafisa wa Israel
Feb 04, 2026 06:53Chama tawala cha African National Congress (ANC) kimemkosoa vikali Mfalme wa Afrika Kusini, Buyelekhaya Dalindyebo kufuatia uamuzi wake tata wa kuwaalika maafisa kutoka Ubalozi wa Israel kutembelea hospitali za umma katika mkoa wa Eastern Cape. Dalindyebo ni mfalme wa watu wa AbaThembu, mojawapo ya jamii kubwa zaidi za kitamaduni za Afrika Kusini.
-
Mashambulizi ya droni yaua watu 15 Kadugli, kusini mwa Sudan
Feb 04, 2026 06:52Raia wasiopungua 15, wakiwemo watoto saba, wameuawa katika mashambulizi ya ndege zisizo na rubani katika mji wa Kadugli kusini mwa Sudan. Hayo yamesemwa na kundi la kujitolea la wenyeji na mashuhuda wa hujuma hiyo ambao wameeleza kuwa, mashambulizi hayo yamejiri saa chache baada ya jeshi la Sudan kutangaza kuvunja mzingiro wa miaka mingi dhidi ya mji wa Kadugli.
-
Droni ya upelelezi ya Iran yakamilisha kazi yake kwa mafanikio katika maji ya kimataifa
Feb 04, 2026 04:03Droni ya doria na ya intelijinsia ya vikosi vya ulinzi vya Iran imefanikiwa kukamilisha kwa mafanikio operesheni yake katika maji ya kimataifa huku ripoti zikiarifu kuwa askari wa Marekani wameitungua ndege moja isiyo na rubani sawa na hiyo.
-
Ripoti ya kila mwaka ya Human Rights Watch: Idadi ya mashahidi waliouawa Gaza inazidi makadirio rasmi
Feb 04, 2026 04:01Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limethibitisha katika ripoti yake ya kila mwaka iliyotolewa leo Jumatano kwamba katika mwaka mzima wa 2025 Israel ilifanya uhalifu wa kivita, uhalifu dhidi ya ubinadamu, vitendo vya mauaji ya kimbari na maangamizii ya kizazi dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza na Ukingo wa Magharibi, na kusababisha vifo, majeraha na kuhamishwa kwa lazima mamia ya maelfu ya watu, kwa kushirikiana na Marekani.
-
Ghannouchi akataa kukata rufaa ya kifungo cha miaka 20 jela kutokana na "ukosefu wa dhamana ya haki"
Feb 04, 2026 03:51Rached Ghannouchi, mkuu wa harakati ya Ennahda na spika wa zamani wa Bunge la Tunisia, alitangaza jana Jumanne kwamba hatakata rufaa mahakamani dhidi ya hukumu ya kifungo cha miaka 20 jela aliyokatiwa katika kile kinachojulikana katika vyombo vya habari kama "Kesi ya Kula Njama - 2," akisema kwamba kesi hiyo haina dhamana ya haki.
-
Duru za Kimataifa: Israel inatumia mrengo wa kulia wa Ulaya kupiga vita Uislamu
Feb 04, 2026 03:50Vyombo vya habari vya kimataifa viimefichua uhusiano unaokua kati ya utawala haramu wa Israel na mrengo wa kulia barani Ulaya, hasa katika kupiga vita Uislamu na Waislamu katika nchi za bara hilo.