Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina amesema kuwa utawala wa Kizayuni wa Israel umeangamiza asilimia 75 ya nyumba, miundombinu ya barabara, vyuo vikuu, misikiti na miundo msingi mingine ya Ukanda wa Gaza.
Polisi nchini Marekani imemtia nguvuni mgombea wa kiti cha urais katika uchaguzi wa mwaka huu nchini humo ambaye alikuwa katika maandamano ya kuiunga mkono Palestina yaliyofanyika katika Chuo Kikuu cha Washington.
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema katika sherehe za ufunguzi wa maonyesho ya sita ya uwezo wa mauzo ya nje ya bidhaa za Iran (Iran Expo 2024) kwamba maonesho haya yanaonyesha kuwa Iran haiwezi kuwekewa vikwazo na ina uwezo wa kufanya uvumbuzi katika nyanja mbalimbali.
Kamishna Mkuu wa Haki za Kibinadamu wa Umoja wa Mataifa ametoa wito wa kufanyika uchunguzi wa kimataifa kuhusu makaburi ya umati yaliyogunduliwa katika hospitali kuu mbili za Ukanda wa Gaza.
Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amewasili katika mji mkuu wa Pakistan Islamabad katika ziara rasmi ya kikazi yenye lengo la kuimarisha usalama na uhusiano wa kibiashara kati ya nchi mbili.
Harakati ya Mapamabano ya Kiislamu (Muqawama) ya Hizbullah ya Lebanon imesema wapiganaji wake wameiangusha ndege ya kisasa isiyo na rubani ya kivita na kijasusi ya utawala haramu wa Israel kusini mwa Lebanon baada ya kukiuka anga ya nchi hiyo.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, Jamhuri ya Kiislamu iliikuwa imeshaitaarifu serikali ya Marekani kabla ya kutekeleza Operesheni ya Ahadi ya Kweli ya kuutia adabu utawala wa Israel mfanyamauaji ya kimbari.
Vyombo vya habari vya utawala wa Kizayuni wa Israel vinazikanusha picha na mikanda ya video inayosambazwa na vyombo kadhaa vya habari, ikionyesha maeneo tofauti ndani ya utawala huo yaliyolengwa na makombora ya Iran ikiwa ni kufuata na kutekeleza sera ya habari ya baraza la mawaziri la vita la utawala huo haramu.
Wananchi konte nchini Iran wamejitokeza mitaani kuunga mkono hatua ya Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) ya kuuadhibu utawala wa Kizayuni wa Israel kufuatia kitendo chake cha kichokozi cha kutekeleza mashambilizi ya kigaidi dhidi ya ubalozi mdogo wa Iran jijini Damascus Aprili Mosi.
Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya ughaibuni ya Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS Khaled Mash'al, amepongeza istiqama ya kishujaa ya Ukanda wa Ghaza na kusisitiza kuwa vita vya miezi sita wanavyopigana Wapalestina na utawala wa Kizayuni wa Israel "karibuni hivi vitamvunja adui Mzayuni".