-
Netanyahu: Ni kweli tuliwaua kigaidi wanasayansi wa nyuklia wa Iran
Jul 13, 2025 03:27Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu amekiri kwamba utawala huo wa Kizayuni uliwaua kwa utaratibu maalum wanasayansi wa nyuklia wa Iran.
-
Maafisa wa Syria na Israel wanatazamiwa kukutana Baku
Jul 13, 2025 02:18Maafisa wa Syria na Israel wanatazamiwa kukutana mjini Baku ili kujadili "uwepo wa hivi karibuni wa jeshi la Israel nchini Syria.
-
Jinai ya kutisha; Israel yaua shahidi Wapalestina 150 Gaza
Jul 13, 2025 02:02Wapalestina zaidi ya 150 wameuawa shahidi katika maeneo mbalimbali ya Ukanda wa Gaza, huku eneo hilo la pwani likishuhudia siku yake mbaya zaidi tangu mwezi Mei, wakati utawala wa Israel uliposhadidisha mauaji yake ya kimbari dhidi ya eneo hilo.
-
Tahadhari kuhusu joto na ukosefu wa maji ya kunywa Gaza
Jul 13, 2025 00:01Shirika la Umoja wa Mataifa la Misaada kwa Ajili ya Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA) limetahadharisha kuhusu hali mbaya ya kiafya huko Gaza Palestina kutokana na ukosefu wa maji ya kunywa na usafi wa mazingira na matokeo ya joto.
-
Raia wa US apigwa hadi kufa na walowezi wa Kizayuni Ukingo wa Magharibi
Jul 12, 2025 09:41Walowezi wa Israel wamempiga hadi kufa kijana mmoja raia wa Marekani katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan unaokaliwa kwa mabavu, kwa mujibu wa familia yake na mashirika ya kutetea haki za binadamu.
-
Wapalestina zaidi ya 17 wauawa katika mashambulizi ya Israel Gaza leo alfajiri
Jul 12, 2025 04:02Kwa mujibu wa ripoti za vyombo vya habari zikinukuu vyanzo vya kitabibu ndani ya Ukanda wa Gaza, Wapalestina wasiopungua 17 wameuawa katika mashambulizi ya anga yaliyofanywa na jeshi la Israel tangu alfajiri ya leo.
-
Lebanon: Hatuna azma ya kuufanya wa kawaida uhusiano wetu na Israel
Jul 11, 2025 12:56Rais Joseph Aoun wa Lebanon amesema nchi hiyo haina mpango wa kuanzisha uhusiano wa kawaida na Israel kwa sasa.
-
Israel yaua mwandishi mwingine wa Kipalestina, idadi ya waliouawa yafika 229
Jul 11, 2025 04:10Ofisi ya serikali ya vyombo vya habari katika Ukanda wa Gaza imetangaza kuwa mwandishi habari mwingine wa Kipalestina ameuawa katika shambulio la Israel katika eneo hilo lililozingirwa kinyume cha sheria, na kuongeza idadi ya wanahabari waliouawa imefika 229 tangu Oktoba 2023, wakati utawala dhalimu wa Israel ulipoanzisha mashambulizi ya kinyama dhidi ya Gaza.
-
Upeo wa ukatili; Israel yaua Wapalestina zaidi ya 80 Gaza ndani ya saa 24
Jul 10, 2025 23:24Mashambulizi ya Israel katika maeneo mbali mbali huko Gaza yameua shahidi watu wasiopungua 82 tangu alfajiri ya jana, kwa mujibu wa Wizara ya Afya ya Gaza, wakati huu ambapo mazungumzo yanaendelea ya kusitisha mapigano hayo.
-
Ansarullah yaionya Israel: Haiyumkiniki kufungua bandari ya Eilat
Jul 10, 2025 17:19Kiongozi wa Harakati ya Ansarullah ya Yemen ametangaza kuwa, ni jambo lisilowezekana kufunguliwa tena kwa bandari ya Eilat (Umm al-Rashrash), akisisitiza msimamo thabiti wa Yemen wa kuendelea kutekeleza vikwazo vya baharini dhidi ya utawala ghasibu wa Israel katika Bahari Nyekundu, Ghuba ya Aden na Bahari ya Arabia.