-
Mjumbe wa UN asema mashambulizi ya anga ya Israel dhidi ya Syria lazima yakome ‘mara moja’
May 03, 2025 22:56Mjumbe Maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Syria, Geir Pedersen, amelaani vikali ukiukaji unaozidi kuongezeka wa mamlaka ya Syria unaofanywa na utawala wa Israel, akisema utawala huo ghasibu lazima usitishe mashambulizi yake ya anga “mara moja.”
-
UNICEF: Watoto wa Gaza wanazidi kujongewa na njaa, maradhi na mauti
May 03, 2025 08:11Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) limeonya kwamba watoto katika Ukanda wa Gaza wanakabiliwa na hatari kubwa ya njaa, magonjwa na vifo, miezi miwili baada ya kukabiliwa na mzingiro wa Israel.
-
Qamati: Ni upuuzi na maneno matupu kutaka Hizbullah ipokonywe silaha
May 03, 2025 08:08Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon imesema kuwa, adui ana hofu kubwa na silaha za muqawama na kwamba, ni maneno ya kipuuzi na yasiyo na maana kutaka harakati hiyo ipokonywe silaha.
-
Khatibu wa msikiti wa al-Aqswa aonya kuhusu siasa hatarishi za wavamizi
May 03, 2025 07:44Khatibu wa Msikiti wa Al-Aqswa ameonya kuhusiana na kushadidi mashambulizi ya Wazayuni dhidi ya Msikiti wa Al-Aqswa na Baytul Muqaddas, na na kutoa mwito wa kukabiliana mara moja na vitendo hivyo visivyo vya kibinadamu.
-
Israel yafanya mashambulio 20 dhidi ya Syria, makali zaidi kushuhudiwa tangu ulipoanza mwaka 2025
May 03, 2025 03:26Duru za habari zimeripoti kuwa, usiku wa kuamkia leo, utawala wa Kizayuni wa Israel umefanya mashambulio yasiyopungua 20 ya anga dhidi ya viunga vya mji mkuu wa Syria Damascus, Dara’a, na Hama yakiwa ndio makali zaidi dhidi ya nchi hiyo tangu ulipoanza mwaka huu wa 2025.
-
Israel yaendeleza mauaji ya kikatili Ukanda wa Ghaza, Yemen yapiga tena
May 02, 2025 22:54Takwimu rasmi zinaonesha kuwa, raia 12 wa Palestina wameuawa shahidi katika mashambulizi ya kikatili ya Wazayuni kwenye maeneo mbalimbali ya Ukanda wa Ghaza hususan katikati mwa ukanda huo. Ukatili huo ulianzia usiku wa manane jana na kuendelea mpaka asubuhi.
-
Lieberman: Kamwe hatuwezi kupata amani Israel
May 02, 2025 22:47Mkuu wa chama cha "Yisrael Beiteinu" amesema kuwa, maadamu utawala unafanya maafa uko madarakani huko Israel, walowezi wa Kizayuni kamwe hawatoonja maisha ya usalama na amani.
-
Yemen yatwanga tena kambi ya anga ya Israel kwa kombora baada ya shambulio la anga la Marekani
May 02, 2025 06:04Msemaji wa Jeshi la Yemen, Brigedia Jenerali Yahya Saree ametangaza kuwa nchi yake imefanya shambulio la kombora dhidi ya kambi ya anga ya jeshi la Israel ili kulipiza kisasi vita vya mauaji ya kimbari vya utawala huo kwenye eneo la Ukanda wa Gaza huko Palestina.
-
Unicef: Watoto wa Gaza wana kiu na wana njaa
May 02, 2025 06:01Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF), limeeleza wasiwasi wake kuhusu hali mbaya waliyonayo watu wa Ukanda wa Gaza, hasa watot na kutaka kukomeshwa kmzingiro dhidi ya ukanda huo.
-
Oparasheni ya kigaidi ya Israel katika maji ya Ulaya; Israel yashambulia meli ya misaada kwa ajili ya Gaza
May 02, 2025 05:56Meli ya Freedom Flotilla, iliyokuwa ikielekea Gaza ilitangaza mapema leo asubuhi kuwa imeshambuliwa na ndege isiyo na rubani ya Israel katika maji ya kimataifa kwenye pwani ya Malta.