Unicef yatahadharisha kuhusu kimbunga cha Mathew
https://parstoday.ir/sw/news/world-i16804-unicef_yatahadharisha_kuhusu_kimbunga_cha_mathew
Mfuko wa Kuhudumia Watoto wa Umoja wa Mataifa (Unicef) umeripoti kuwa watoto zaidi ya milioni nne nchini Haiti wanakakabiliwa na hatari ya uharibifu iliyosababishwa na kimbunga cha Mathew kilichoathiri visiwa vya eneo la Caribean.
(last modified 2023-11-27T12:14:11+00:00 )
Oct 05, 2016 14:59 UTC
  • Unicef yatahadharisha kuhusu kimbunga cha Mathew

Mfuko wa Kuhudumia Watoto wa Umoja wa Mataifa (Unicef) umeripoti kuwa watoto zaidi ya milioni nne nchini Haiti wanakakabiliwa na hatari ya uharibifu iliyosababishwa na kimbunga cha Mathew kilichoathiri visiwa vya eneo la Caribean.

Marc Vincent Mwakilishi wa Shirika la Unicef nchini Haiti  ameeleza kuwa hicho ni kimbunga kibaya zaidi kuwahi kushuhudiwa huko Haiti katika miongo ya hivi karibuni na kwamba madhara yake bila shaka yatakuwa makubwa. Mwakilishi wa Unicef nchini Haiti ameongeza kuwa magonjwa yanayosababishwa na kuchafuka maji ni tishio la kwanza litalowakabili watoto katika mazingira ya sasa baada ya kimbunga hicho na kwamba shirika hilo linatoa kipaumbele kwa suala la kuwadhaminia watoto wa nchi hiyo maji ya kutosha.

Hali ya mambo wiki hii huko Port au Prince maji mkuu wa Haiti kufuatia kimbunga cha Mathew

Katika hali ambayo Haiti ingali ipo katika marhala ya kujijenga upya baada ya kuathiriwa na tetemeko la ardhi mwaka 2010, raia elfu 55 wa nchi hiyo wangali wanaishi katika makazi ya muda huku asilimia 40 ya wengine wakitumia maji yasiyo salama katika maisha yao ya kila siku. Kimbunga cha Mathew ambacho kinakwenda kwa kasi ya karibu kilomita 215 kwa saa tayari kimefika katika pwani ya mashariki mwa Cuba baada ya kusababisha madhara huko Haiti.