Mshukiwa mkuu wa mashambulizi ya kigaidi Barcelona auawa
https://parstoday.ir/sw/news/world-i33468-mshukiwa_mkuu_wa_mashambulizi_ya_kigaidi_barcelona_auawa
Polisi ya Uhispania imemuua Younes Abouyaaqoub aliyetekeza shambulio la kigaidi la Alkhamisi wiki iliyopita katika mji wa Barcelona.
(last modified 2026-02-21T22:51:18+00:00 )
Aug 21, 2017 22:52 UTC
  • Mshukiwa mkuu wa mashambulizi ya kigaidi Barcelona auawa

Polisi ya Uhispania imemuua Younes Abouyaaqoub aliyetekeza shambulio la kigaidi la Alkhamisi wiki iliyopita katika mji wa Barcelona.

Vyombo vya habari vya Uhispania vimetangaza kuwa, mshukiwa huyo alipigwa risasi eneo la Subirats, karibu na Sant Sadurní d'Anoia lililoko umbali wa kilomita 60 kutoka Barcelona na alionekana kuvaa mkanda wa kujilipua.

Polisi wamethibitisha kwamba mshukiwa huyo ni Younes Abouyaaqoub, 22, ambaye awali alikuwa akisakwa kuhusiana na shambulio hilo la Las Ramblas.

Abouyaaqoub alikuwa akisakwa na polisi ya Uhispania tangu Alkhamisi iliyopita baada ya kuua watu 13 kwa kuwakanyaga kwa makusudi kwa gari katikati ya mji mwa Barcelona na kutoroka.

Huduma ya kwanza kwa wahanga wa shambulizi la kigaidi, Barcelona

Baada ya mauaji ya watu katika mtaa wa Las Ramblas, Younes Abouyaaqoub aliteka gari jingine baada ya kumdunga kisu na kumuua dereva wake na kutoroka nalo hadi alikouliwa mafichoni.

Polisi ya Uhispania imetangaza kuwa, ingali inawasaka washukiwa wengine waliohusika na mashambulizi mawaili ya wiki iliyopita katika mji wa Barcelona. Watu 15 waliuawa katika mashambulizi hayo.

Kundi la kigaidi la Daesh limetangaza kuwa, ndilo lililopanga mashambulizi hayo.